Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MBUNGE AWAONYA WALIOVAMIA NA KUJENGA MAENEO YA WAZI,AWATAKA KUONDOKA MARA MOJA

TANGAZO

Na Christopher Lilai,Liwale.
Mbunge wa jimbo la Liwale mkoani Lindi,CUF,Zuberi Kuchauka,amewataka wale wote waliovamia maeneo ya huduma za jamii yakiwemo maeneo ya zahanati na shule  kuondoka mara moja.

Agizo hilo amelitoa hivi karibuni alipotembelea kijiji cha  Mpengele,kata ya Makata kukagua eneo la zahanati ambalo limevamiwa na wafanya biashara huku akiwataka viongozi wenye tabia ya kushiriki kuhujumu maeneo hayo kuchukuliwa hatua za kisheria.

Kuchauka ambaye alikuwa kwenye ziara ya kwanza mara baada ya kuapishwa  alisema kila kijiji kilitenga maeneo kwa ajili ya  huduma za kijamii hivyo ni vyema viongozi wakayalinda na kuhakikisha hayavamiwi kwa maslahi ya mtu binafsi.

“Kila kijiji kina maeneo yametengwa kwa ajili ya makazi na shughuli za kijamii ni vizuri yakaheshiwa kwa maslahi ya umma na si maslahi binafsi”alisema Kuchauka.

Alimtaka Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo kufanya uhakiki wa maeneo yote ya huduma za kijamii yaliyovamiwa ili hatua  zichukuliwa kwa wale watakaobainika wamehusika na ugawaji kiholela au kuvamia.

Aidha alimtaka Mkurugenzi mtendaji huyo kuhakikisha maeneo yote ya umma  yakiwemo ya mijini na  vijijini yanapimwa na yanapatiwa hati za kumiliki kisheria ili kuepuka  migogoro isiyo na lazima.

Kwenye kijiji cha Mpengele,serikali ya kijiji hicho umeingia mgororo mkubwa kati yao na mfanyabiashara na mkazi wa kijiji  hicho Kaimu Mkungu ambaye amejenga ndani ya eneo la zahanati ambapo licha ya kutakiwa kuondoka amekuwa anagomea  kwa kudai kuwa eneo hilo alipatiwa na uongozi wa kijiji hicho tangu mwaka 2006.


Kuchauka pia amemwagiza afisa Mtendaji wa kata ya Makata,Chande Kilemba kuingilia kati mgogoro huo ili eneo hilo liendelee kuwa chini ya mmiliki halali ambae ni serikali ya kijiji cha Mpengele.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top