Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

KABILA LA WAMWERA WANAVYOENDELEZA MILA NA DESTURI ZAO ZA JANDO NA UNYAGO

TANGAZO
Na Chillumba Clarence,Malolo-Ruangwa.
Kila mwaka inapofika mwezi juni baada ya shule za msingi kufungwa katika wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi Tz, yenye wenyeji wa asili wa kabila la Wamwera kunakuwa na mila na desturi ya jando kwa watoto wa kiume na unyago kwa watoto wa kike ingawa kwa miaka ya hivi karibuni utaratibu huo wa kufanya shughuli hizo kila mwaka umevurugika na hii ni kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa yanayoambatanana na ukame unaosababisha njaa.
Katika mila na desturi hizo kwa kabila la Wamwera watoto hupelekwa jandoni ambako hupewa elimu ya namna ya kukabiliana na mazingira yao pindi wanaporejea kutoka kwenye mafundisho hayo.
Pichani chini,ni baadhi ya matukio yaliyojiri wakati wa sherehe hizo zilizofanyika Julai 7&8 2015 katika kijiji cha Malolo wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi ambako maelfu ya wananchi walijitokeza kushiriki shughuli hizo muhimu katika kabila la Wamwera.
 WAZAZI na Marafiki wakiwa wamewabeba watoto wao wakielekea Kanisani kwa ajili ya kushiriki misa ya shukrani ya watoto wao baada ya kukaa kwa muda wa mwezi mmoja wakiwa jandoni ambako hufundishwa mambo mbalimbali kuhusu maadili mema.
 JENGO ambalo watoto wa kike huwekwa katika kipindi chote cha unyago maarufu (Chiputu) ambalo hujengwa kwa mabua ya mazao ya mtama au Mahindi na kuezekwa kwa nyasi watoto hao hukaa katika jengo hilo kwa kipindi kisichozidi mwezi mmoja kabla ya kuchukuliwa na wazazi wao siku ya kurudi nyumbani siku ambayo wamwera huiita –Chianguro,siku ambayo hufanyika sherehe kubwa inayoambatana na burudani za ngoma za asili.

BAADHI ya wazazi wa watoto wakicheza ngoma wakiwa chini kuashiria furaha isiyo na kifani kurejea nyumbani kwa watoto wao wa kike na kiume ambapo watoto wa kike huitwa unyago na kwa watoto wa kiume huitwa Jando. Lengo kuu la mila hizo ni kumpa mtoto elimu ya maisha na mahusiano yake na jamii inayomzunguka.
JENGO ambalo watoto wa kiume hukaa wakiwa jandoni kwa kipindi cha mwezi mmoja au zaidi likiwa limeteketezwa kwa moto ikiwa ni ishara kuwa tayari siku za watoto hao wa kiume kukaa hapo jandoni zimeisha na hatimaye kurudi nyumbani kukutana nao tena wazazi wao.Sehemu hii wamwera wanaiita-Likuta na siku jengo hilo linapochomwa moto wamwera huimba wimbo “Amwali….Mwali..kwa…Mwali…Kwa…Mwali…KwaX2.. Kumishonjo Kupile Moto” Tafsiri ya wimbo huo…mwanamke ulikuwa wapi? Tayari kule jandoni kumeungua moto.
 WATOTO waliotoka jandoni wakiogeshwa na ndugu,jamaa na marafiki siku ambayo huitwa “Chianguro” ambapo baada ya shughuli hiyo ya kuogeshwa watoto hao huveshwa nguo Mpya kuashiria kuwa tayari wako katika ulimwengu mpya ambao wanakuwa tofauti kimaadili na watoto wenzao waliowaacha nyumbani. Katika tukio hilo baadhi ya ndugu hulala chini na watoto hao huwa juu yao pindi wanapoogeshwa.
 WATOTO na Wazazi wakiwa kanisani katika misa ya shukrani ambayo hufanyika kila mwaka kunapokuwa na shughuli hizo za jando na unyago katika kanisa katoliki la Mtakatifu Joseph Parokia ya Malolo,Kigango cha Malolo,Jimbo la Lindi. Baada ya misa hiyo ndipo watoto hutoka nje na kuelekea uwanjani ambako hufanyika shughuli mbalimbali ikiwemo uchezaji wa ngoma za asili maarufu Likomanga na Shikundumbwi.
 WAZAZI na ndugu wakiwa wamewabeba watoto wao mabegani wakitoka kanisani wakiwa wamevalishwa nguo mpya na mikononi mwao wakiwa wameshika miavuli hiyo yote ni ishara kuwa tayari watoto hao wanakuwa wameingia kwenye furaha ya siku hiyo ya Chianguro.
 WAZAZI na ndugu wakiwa wamewabeba watoto wao mabegani wakitoka kanisani wakiwa wamevalishwa nguo mpya na mikononi mwao wakiwa wameshika miavuli hiyo yote ni ishara kuwa tayari watoto hao wanakuwa wameingia kwenye furaha ya siku hiyo ya Chianguro.
 WAZAZI wakicheza kwa furaha wakiwa kwenye uwanja ambao huandaliwa kwa shughuli hiyo na mara baada ya sherehe za hapo uwanjani (Luwala) watoto hao hupelekwa nyumbani ambako nako sherehe hizo huendelea kufanyika.

WATOTO hao wakiwa wamebebwa mabegani mwa wazazi wao tayari kupelekwa nyumbani kwao kwa ajili ya kuendelea na sherehe zingine katika kufurahia mila na Desturi za kabila la Wamwera linalopatikana mkoani Lindi.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top