Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

Taarifa Mpya Ya Mlipuko Wa Homa Ya Mapafu Ya Ng'ombe Halmashauri Ya Mji Wa Masasi.

TANGAZO
Picha ya Ng'ombe

TAARIFA YA MLIPUKO WA HOMA YA MAPAFU YA NG’OMBE
Ndugu wananchi wa mji wa Masasi na vitongoji vyake taarifa iwafikie kwamba katikakati ya mwezi Februari 2016, kumetokea mlipuko wa Homa ya mapafu ya Ng’ombe (Contagious Bovine Pleuropneumonia) katika kijiji cha Mkarango Halmashauri ya mji wa Masasi.

Aidha hadi Machi 01, 2016 jumla ya Ng’ombe 18 waliripotiwa kufa kutokana na ugonjwa huo katika kijiji hiko cha Mkarango.

Ugonjwa huu ni hatari sana na kwamba unaambukizwa kwa kasi kubwa ambapo wanyama wote jamii ya Ng’ombe (Bovine) wakiwemo Ng’ombe,Nyati,na Nyati Maji huathiriwa na ugonjwa huu.

Ugonjwa huu wa mapafu ya Ng’ombe unaambukizwa kwa njia ya mafua kutoka kwa wanyama wanaougua lakini pia huambukizwa kwa njia ya mate kwa kuchangia chakula na maji yaliyochafuliwa na vijidudu vya ugonjwa huo.
Hivyo basi kutokana na kushambuliwa na kuathirika kwa njia ya hewa wanyama wengi walioathirika na ugonjwa huo hufa.

DALILI ZA UGONJWA
·        Mnyama hupumua kwa shida na kukohoa.
·        Mnyama hutokwa na mafua
·       Mnyama hupoteza hamu ya kula na kuonekana kujitenga kutoka kundi kubwa.
·     Mnyama aliyekufa akipasuliwa sehemu ya kifua huonekana ikiwa imejaa maji ya rangi ya njano.
·     Mapafu huonekana yakiwa yamevimba na kubadilika rangi kama ya maini pia yanaonekana yakiwa yameganda kwenye mbavu na kufunikwa na ute mzito wa njano.
CHANJO NA TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba yeyote ukishatokea bali chanjo ya kuzuia ugonjwa huo inatakiwa itolewe miezi kadhaa kabla ugonjwa haujatokea.
Kufuatia kujiridhisa kwetu kwamba ugonjwa huo upo baada ya taarifa kutoka kwa wafugaji wa kijiji cha Mkarango,tumepeleka taarifa mkoani pia kwenye kituo cha uchunguzi wa magonjwa ya mifugo (VIC) Naliendele kwa hatua zaidi za utekelezaji ili kunusuru kundi la ng’ombe takribani 500 wa kata za Temeke,Migongo na Mwenge Mtapika lililo katika hatua ya kuambukizwa.

NB:
Nyama ya mgonjwa aliyekufa kwa ugonjwa haina madhara yoyote kwa binadamu.

Clarence Antony Chilumba,
Ofisa Habari Halmashauri ya mji wa Masasi
S.L.P. 447,
MASASI.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top