Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

VIONGOZI WAKUU EAC,SADC,EU WAALIKWA KUSHUHUDIA TUKIO LA KIHISTORIA LA KUAPISHWA KWA MAGUFULI

TANGAZO
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakifanya mazoezi katika Uwanja wa Uhuru jana ikiwa ni matayarisho kwa ajili ya hafla ya kuapishwa kwa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli itakayofanyika uwanjani hapo keshokutwa.

Viongozi Wakuu kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), na wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc), wamethibitisha kuhudhuria sherehe za kumuapisha Rais Mteule, Dk. John Magufuli keshokutwa jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na Nipashe kuhusu maandalizi ya kuwapokea wageni mbalimbali kutoka nje ya nchi wanaotarajia kuhudhuria sherehe hiyo.

“Mialiko imeshakwenda, lakini mpaka sasa hakuna aliyewasili, ila tumeshaanza kupokea majibu ya viongozi mbalimbali wa kanda kuwa watafika katika sherehe hiyo,” alisema Balozi Mulamula.

Alisema nchi jirani kama Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Uganda, zimethibitisha kushiriki sherehe za kumuapisha Dk. Magufuli. Alisema orodha kamili na idadi ya wageni watakaokuja, bado haijapatikana, lakini Wizara imeshajiandaa kupokea idadi yoyote ya wageni watakaokuja.

Alisema licha ya Ofisi ya Waziri Mkuu kusimamia sherehe hiyo, lakini Wizara nayo imejipanga katika suala zima la malazi kwa wageni watakaofika nchini.

Aliongeza kuwa pia wanatarajia kupokea wageni kutoka China, nchi za Nordic, Marekani na Uholanzi.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top