Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

IDADI YA MAHUJAJI WA TANZANIA WALIOFARIKI KWA MKANYAGANO WAKATI WA HIJJA MAKKA YAFIKIA 11

TANGAZO
Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeir Bin Ally (picha ya maktaba)

SERIKALI imepokea majina matatu ya mahujaji wengine wa Tanzania, waliokufa kutokana na tukio la kukanyagana lililotokea eneo la Mina, katika mji Mtakatifu wa Makka, Saudia Arabia Septemba 24, mwaka huu, hivyo kufanya idadi ya mahujaji wa Tanzania waliopoteza maisha nchini humo kufikia 11.
Hayo yalithibitishwa jana na Serikali kupitia taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari. Taarifa hiyo iliwataja watatu zaidi waliokufa kuwa ni Yusuf Ismail Yusuf kutoka kikundi cha Khidmat Islamiya, Rahma Salim Suweid kutoka kikundi cha Ahlu Daawa na Issa Amir Faki.
Ilisema mahujaji hao walitambuliwa baada ya kupitia taarifa zao za vidole zilizotolewa na Serikali ya Saudi Arabia. Serikali ilisema vifo hivyo vinaendelea kuwa pigo kwa taifa na kwamba, vimepokelewa kwa masikitiko makubwa.
“Aidha, Ubalozi unaendelea kushughulikia taratibu za maziko kwa mahujaji ambao wamefariki dunia na miili yao kutambuliwa. Tunapenda kufafanua kuwa mali za marehemu ikiwemo mizigo waliyokuwa nayo wakati wa Hijah zitawasilishwa nyumbani Tanzania na vikundi walivyokuja navyo na kukabidhiwa kwa jamaa wa marehemu,” ilieleza wizara.
Pia ilieleza kuwa Ubalozi unaendelea kufuatilia orodha mpya ya taarifa za vidole, iliyotolewa na Serikali ya Saudi Arabia kwa ajili ya kuwabaini mahujaji wa Tanzania ambao hawajatambuliwa. Mpaka sasa zaidi ya mahujaji 30 wa Tanzania hawajulikani walipo.
CHANZO:HABARI LEO.



TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top