Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

NEC,JESHI LA POLISI NA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA WILAYA WAKUBALIANA KUTENDA HAKI UCHAGUZI MKUU

TANGAZO
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji mstaafu Damian Lubuva.


MWENYEKITI wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Damian Lubuva, amewataka   makamanda wa polisi wa Mikoa ya Tanzania bara pamoja na Zanzibar na mawakala wa uchaguzi kuhakikisha  wanatenda  haki ili uchaguzi wa mwaka huu uwe wa uhuru, amani na  haki.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Jaji Lubuva, alisema kosa dogo linaweza kuleta uvunjifu wa amani katika uchaguzi huo hivyo tume imeamua kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kuwapata uelewa kuwezesha utekelezaji wa  majukumu yao katika uchaguzi mkuu.

Alisema katika chaguzi zilizo pita Tume ilikua ikifanya mikutano tofauti ambapo ilikuwa inakutana na watendaji wa uchaguzi peke yake na makamanda wa polisi peke yake, hivyo mkutano wa mwaka huu ni tofauti na mikutano iliyopita.

Jaji Lubuva alisema ili uchaguzi uwe wa huru na haki ni lazima uendeshwe katika hali ya utulivu na amani na hali ya usalama  ili kuwezesha wapiga kura kutumia haki yao ya kikatiba kwa kwenda vituoni kupiga kura bila ya kuwa na hofu.

"Jeshi la polisi lina jukumu la kuhakikisha hali ya usalama na amani katika kipindi cha uchaguzi ndiyo maana Tume imeamua kushirikiana Jeshi la Polisi kulinda amani," alisema Jaji Libuva.

Alisema wadau hao wote wana jukumu la kusimamia zoezi hilo zima ili liweze kumalizika kwa usalama, kwani kosa moja linaweza kusababisha uvunjifu wa amani katika maeneo mbalimbali ya nchi.

"Ni muhimu kufanya kazi zenu kwa weledi mkubwa,uadilifu na kwa kufata sheria,kanuni na taratibu za uendeshaji uchaguzi kama ilivyoelekeza na Tume ya Uchaguzi," alisema Jaji Lubuva.

Jaji Libuva alisema katika chaguzi zilizopita kulikuwepo na changamoto ya makundi ya vijana wanaohisiwa kuwa wafuasi wa vyama vya siasa kwa kuwatishia wapigakura hususani akinamama ili wasiende kupiga kura,ambapo hilo linawasababishia watu kukosa haki ya msingi ya kupiga kura.

Naye Inspekta wa Polisi (IGP) Ernest Mangu, alisema watahakikisha uchaguzi unaenda kwa amani bila kuleta madhara kwa wapiga kura.Alisema hawataruhusu mpiga kura kubaki katika vituo vya kupigia kura kwani mawakala wa kila chama wana jukumu la kulinda kura za vyama vyao.

Aliongeza kuwa kila mdau analo jukumu la kufanya kazi na kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika katika mazingira ya amani na utulivu.  

TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top