Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

ASKOFU ANGELUS MCHOMANJOMA WA KANISA LA PENTEKOSTE AWATAKA WATANZANIA KUILINDA AMANI.

TANGAZO

Na Clarence Chilumba,Masasi.
Askofu wa kanisa la Sayuni International Pentekoste, Masasi mkoani Mtwara Angelus Mchomanjoma  amewataka Watanzania kuilinda amani iliyopo ambayo ni tunu kwa taifa letu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu oktoba 25 mwaka huu.

Wito huo ameutoa jana wakati anaongea na "Blog ya Mtazamo Mpya" kuhusu maandalizi ya tamasha la kuombea amani mkoa wa Mtwara litakalofanyika oktoba 11, 2015 kwenye viwanja vya Boma mjini Masasi.

Alisema lengo kuu la tamasha hilo ni kuombea amani ili matokeo ya uvunjifu wa amani yasijitokeze kipindi hiki cha kampeni na baada ya matokeo kutangazwa na kwamba Rais atakayechaguliwa na hatimaye kutangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi ndie chaguo la mungu.

Alisema tamasha hili la kuombea amani mkoani Mtwara ambalo litashirikisha maaskofu,wachungaji pamoja na waimbaji kutoka kwenye kwaya mbalimbali za makanisa hayo ya kipentekoste kutoka ndani na nje ya mkoa wa Mtwara litaanza majira ya saa 8:00 mchana na kumalizika 12:30 jioni.

Kwa mujibu wa askofu huyo alisema tamasha hilo linakuja kwa kuzingatia matokeo ya uvunjifu wa amani yaliyotokea mkoani Mtwara ambayo kwa kiasi kikubwa yaligharimu maisha na mali za wananchi na kusababisha hasara kubwa ya mamilioni ya fedha.

“Tamasha hili si la kunadi sera za wagombea…na ninatoa wito kwa wananchi wote na hata wagombea ambao tumewaalika watakaohudhuria kutovaa sare za vyama vyao vya  siasa na pia tumewaelekeza kutoshangilia kwa kuonesha ishara ya vyama vyao vya siasa”alisema Mchomanjoma.

Alisema tamasha hilo lenye lenye kauli mbiu ya “umoja wetu ndio msingi wa amani yetu” ni sehemu muafaka kwa maaskofu na wachungaji wa umoja wa makanisa ya kipentekoste kuhubiri neno la mungu kwa ajili ya kulinda na kuitetea amani kipindi chote cha uchaguzi.

Akizungumzia kuhusu ulinzi alisema tayari wameshawasilisha maombi kwa mkuu wa jeshi la polisi wilaya ya Masasi na kwamba ni matumaini yao kuwa ulinzi utaimarishwa huku akiwataka wananchi wa wilaya ya Masasi na mkoa wa Mtwara kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kwani hakutakuwa na kiingilio.

Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Kanisa, alisema haoni mantiki ya baadhi ya wanasiasa wanaotafuta kuchaguliwa kwa kuwaahidi Watanzania kuwapatia huduma bure,kama za afya,elimu na maji;badala ya kuwahimiza wafanye kazi ili kujiinua kiuchumi.

Tamasha hilo la kuombea amani mkoa wa Mtwara limeandaliwa na askofu Mchomanjoma kwa ushirikiano na umoja wa makanisa ya pentekoste mkoani humo huku maaskofu,wachungaji na kwaya mbalimbali zikialikwa.



TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top