Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

WATANZANIA WAKUMBUSHWA UMUHIMU WA KULINDA NA KUITUNZA AMANI KATIKA UCHAGUZI MKUU UJAO

TANGAZO
Askofu wa kanisa katoliki jimbo la Lindi Mhashamu Bruno Ngonyani

Na Clarence Chilumba,Mtwara.
Askofu wa kanisa katoliki jimbo la Lindi Mhashamu Bruno Ngonyani amewataka Watanzania kudumisha amani iliyopo kwa kuchagua viongozi wenye uadilifu na watakaotenda haki na usawa kwa watanzania wote.

Wito huo ameutoa wakati anaongoza Ibada ya kufunga mwaka kwa familia za kikristo iliyofanyika kwenye viwanja vya chuo kikuu cha SAUTI tawi la Mtwara  na kuhudhuriwa na waumini wa kanisa hilo kutoka kwenye majimbo saba yanayounda kanda ya kusini,mwishoni mwa juma hili.

Alisema amani ni kitu muhimu kwa ustawi wa Taifa na kwamba amani hiyo hutoweka pindi yanapotokea machafuko huku waathirika wakubwa wa machafuko hayo wakiwa ni akinamama pamoja na watoto.

Alisema mwaka huu ni wa kipekee katika historia ya siasa za Tanzania kwani wananchi wa rika mbalimbali wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kushiriki kwenye mikutano ya kampeni huku akiwaomba kuchagua kiongozi yule ambaye atakuwa na sera nzuri kwa taifa.

“Wananchi mnapaswa kupima ahadi zinazotolewa na wagombea wa vyama vyote vya siasa kama zinatekelezeka au hazitekelezeki ili siku ya kupiga kura mfanye maamuzi sahihi kwa kumchagua kiongozi aliyetoa ahadi zinazotekelezeka”.alisema Ngonyani.

Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Kanisa, aliwaomba wananchi wenyewe watendeane haki huku akiiomba serikali pia kutenda haki kwa raia wake katika kipindi hiki cha uchaguzi kwa kuwa ni jukumu la serikali kutenda haki kwa raia wake.

Kwa upande wake kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara Johansen Bukwali alisema jambo muhimu ni kudumisha familia na  amani kwa kutii utawala uliopo na kutekeleza kanuni zilizopo ili uchaguzi uwe huru na wa amani kwani baada ya uchaguzi maisha yanaendelea.

Maadhimisho hayo ya mwaka wa familia yalitangazwa na kanisa katoliki septemba 27,2014 ambapo kwa kanda ya kusini yalifanyika jimbo la Mtwara na kuhudhuriwa na majimbo ya Songea,Iringa,Tunduru-Masasi,Mbeya,Njombe, pamoja na jimbo la Mbinga.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top