Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

JESHI LA POLISI MKOANI MTWARA LAKANUSHA TAARIFA ZA KUKAMATWA KWA MASANDUKU YA KURA MASASI

TANGAZO
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mtwara  ACP Henry Mwaibambe

Na Fatuma Maumba: Mtwara.
JESHI la Polisi Mkoani Mtwara,limekanusha taarifa iliyotolewa jana Septemba, 29 mwaka huu majira ya  saa 8: 00 mchana kwenye mtandao wa kijamii wa “Jamii Forum” iliyoandikwa kuwa kituo cha Polisi wilaya ya Masasi mkoani humo wamekamatwa watuhumiwa wawili wakiwa na masanduku ya kupigia kura na fomu za kupigia kura zipatazo elfu mbili zikiwa tayari zimetumika na kumpa alama ya vema mgombea wa Urais kupitia chama cha mapinduzi CCM Mhe. John Pombe Magufuli na mbunge wa CCM jimbo la Masasi Mwalimu Rashidi Chuachua.

Akizungumza leo na waandishi wa habari ofisini kwake,Kamanda wa polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Henry Mwaibambe, amesema mtandao huo umeandika kwamba  watuhumiwa hao baada ya kufika kituo cha polisi Mkuu wa wilaya ya Masasi,Bernald Nduta, aliingilia kati na kulazimisha  watuhumiwa hao waachiwe kwa dhamana kwa amri ya mkuu huyo wa wilaya kitu ambacho si cha ukweli ni cha upotoshaji.

“Taarifa hizi ni za uongo na hazina chembe yeyote  ile ya ukweli…hata mimi nashangaa taarifa hizi zinatoka wapi taarifa hizi hazina lengo zuri kwa watanzania hususani kwa wananchi  wa mkoa wa Mtwara nahaidi tutamtafuta  kwa juhudi zetu zote huyo mtu aliyetoa taarifa hizi na kwamba jeshi la polisi linasikitika sana”.alisema Mwaibambe.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara amesema  hakuna Mtu wala watu ambao wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kosa la kukutwa na masanduku ya kura na karatasi za kupigia kura huo ni uzushi na uvumi tu na kwamba hakuna  ukweli wowote lengo ni kupotosha jamii.

 “Ndugu zangu wanahabari nyinyi ni mashuhuda kuwa hivi karibuni mwenyekiti wa tume ya Taifa ya uchaguzi Jaji mstaafu Damiani Lubuva alisema mbele ya waandishi wa habari kuwa masanduku ya kupigia kura  kutoka Afrika ya kusni yataanza kuwasili nchini mwishoni mwa mwezi huu na yatasambazwa mikoani sasa sijui watu hawa wana nia gani kwa Taifa letu”.alisema Mwaibambe.

Aidha  amewaomba wananchi mkoani Mtwara na Tanzania kwa ujumla  kuwa katika kipindi hiki cha uchaguzi si vizuri kuwapa hofu  isiyostahili watanzania,si vizuri kuwapa watanzania mambo ambayo si ya kweli kwani kwa kufanya hivyo ni kujenga chuki kwa vyombo vya usalama na tume ya taifa ya uchaguzi ili wananchi waamini kuwa masanduku ya kupigia kura tayari yapo hapa nchini.

Amesema hadi sasa kampeni za uchaguzi mkoani humo zinaendelea vizuri licha ya kukiri kuwa ziko baadhi ya changamtoo ambazo amehaidi kuzishughulikia ikiwemo taarifa za kuwa baadhi ya wagombea kuwaambia wanaume kuwa kama wameoa basi siku ya kupiga kura wafiche kadi za wake zao ili wasiende kupiga kura kumchagua kiongozi wanayemtaka.

Kamanda Mwaibambe licha ya kuzungumza na  waandishi wa habari  pia ametoa waraka wa septemba 30 mwaka huu kwa waandishi wa habari wenye taarifa ya kukanusha uvumi huo uliowastua wananchi wa mji wa Masasi na mkoa wa Mtwara kwa ujumla.




TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top