Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

BONANZA LA MICHEZO LAFANYIKA MASASI,WAKURUGENZI WAOMBWA KUIPA KIPAOMBELE SEKTA YA MICHEZO

TANGAZO
 kikosi cha Timu ya watumishi wa idara mbalimbali katika Halmashauri ya wilaya ya Masasi ambayo ilishiriki mchezo wa mpira wa miguu katika bonanza maalumu lililofanyika kwenye viwanja vya sekondari ya Ndanda mwishoni mwa wiki.


Na Clarence Chilumba, Masasi.
MKURUGENZI mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Beatrice Dominick amewaomba wakurugenzi wa halmashauri pamoja na taasisi zingine nchini kutekeleza kwa vitendo sera ya elimu kuhusu michezo ili kudumisha ushirikiano miongoni mwa watendaji wa serikali.

Aliyasema hayo jana wakati anafanya mahojiano maalumu na habari leo kwenye uzinduzi wa bonanza la michezo lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya sekondari Ndanda ambapo alisema lengo la bonanza hilo ni kundeleza mahusiano ya kada mbalimbali kwenye halmashauri hiyo.

Katika bonanza hilo kuwahi kutokea kwa siku za hivi karibuni wilayani Masasi liliwashirikisha wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri hiyo,maofisa watendaji wa kata tano  zilizo jirani na shule hiyo,wanafunzi,walimu pamoja na watumishi  wa shule ya sekondari ya Ndanda huku michezo mbalimbali ikishindaniwa.

Alisema bonanza hilo ni mwanzo mzuri kwao kwani hata wale watumishi ambao kwa namna moja ama nyingine walitofautiana wakiwa kazini walipata muda wa kushirikiana pamoja kwenye michezo mbalimbali na kwamba kwa kufanya hivyo ni dhahiri bonanza hilo limesaidia kuzika rasmi tofauti za baadhi ya watendaji wa halmashauri hiyo.

 Mgeni rasmi katika Bonanza la michezo la watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Masasi ambaye ni Ofisa wa Kikosi cha kuzuia na kupambana na Rushwa wilaya ya Masasi Bw.Nestory Gatawa(kulia) akimkabidhi kikombe mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Masasi Beatrice Dominick kwenye bonanza hilo.

KAMANDA wa kikosi cha kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU wilaya ya Masasi Nestory Gatawa akizungumza wakati anafunga bonanza la michezo lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya sekondari ya Ndanda.

Akizungumza kamanda wa kikosi cha kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) wilaya ya Masasi Nestory Gatawa alisema wadau wa michezo wanapaswa kuiga mfano uliooneshwa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Masasi kwa kufanya matamasha na mabonanza ya michezo yenye lengo la kuimarisha ushirikiano.

Alisema kupitia bonanza hilo watendaji wa serikali wa halmashauri hiyo wamepata fursa ya kuwa pamoja na maofisa kadhaa wa Takukuru wilayani humo huku akikiri kuwa watendaji wengi wa serikali wamekuwa na dhana kuwa Takukuru ni maofisa ambao hupaswi kuwa nao karibu.

Kwa mujibu wa Gatawa alisema Takukuru ni kama taasisi zingine za serikali na kwamba watendaji wa serikali na wananchi waondoe hofu na mashaka juu ya taasisi hiyo huku akisisitiza kuwa michezo nao husaidia harakati za kupoambana na rushwa kwa kutoa elimu kupitia klabu za wapinga rushwa zilizopo mashuleni.

 Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye bonanza hilo la michezo na hapa ni mchezo wa kunywa soda kwa haraka.

Kwa upande wake mkuu wa shule ya sekondari ya Ndanda Morega Mongate ambaye ndiye muandaaji wa bonanza hilo alisema serikali imekuwa ikihimiza michezo mashuleni katika kutekeleza dhana nzima ya michezo mashuleni iliyopo kwenye sera ya elimu ili kuibua vipaji vya michezo nchini.

Alisema licha ya changamoto ya rasilimali fedha iliyopo kwenye shule nyingi nchini lakini wakuu wa shule wanapaswa kuwa wabunifu katika kuhakikisha wanapata fedha za kuandaa mabonanza kama hayo kwa kuwa kupitia michezo wanafunzi hupata fursa ya kujifunza masuala mbalimbali ya msingi ikiwemo kudumisha ushirikiano.


Aidha aliwaomba wakuu wa shule nchini kuwa na mpango maalumu kuhusu michezo ili wanafunzi waweze kushiriki kikamilifu katika michezo mbalimbali huku akitiolea mfano kuwa katika shule yao wamekuwa na utaratibu wa kuandaa mashindano ya mabweni, madarasa pamoja nay a kutafuta vipaji vya wanafunzi katika michezo mbalimbali.


 Ofisa elimu sekondari Halmashauri ya wilaya ya Masasi Paula Nkane (kushoto) akicheza mchezo wa "MDAKO' na Ofisa elimu Msingi wa Halmashauri ya wilaya ya Masasi Bi.Editha Fue wakati wa bonanza la michezo lililofanyika huko Ndanda mwishoni mwa wiki.



Mwalimu Jane Mbunda ambaye ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi Njenga halmashauri ya wilaya ya Masasi alikuwa ni miongoni mwa washiriki wa bonanza hilo alisema amefarijika kushiriki kwenye bonanza hilo kwani limesaidia kujenga mahusiano mazuri sambamba na kuimarisha afya za watumishi wa halmashauri hiyo.




 Timu za mpira wa miguu zikiwa zinajiandaa kabla ya kuanza mchezo huo.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top