Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

ASKOFU AHIMIZA WATANZANIA KUFANYA KAZI BADALA YA KUTEGEMEA MISAADA KUTOKA KWA MATAJIRI

TANGAZO
 PADRE Plasidus Mtunguja (aliyeshika  fimbo ya kiaskofu) mara baada ya kutawazwa kuwa Abate wa kwanza mwananchi na ni Abate wa tano tangu shirika la Mtakatifu Benedikto lije eneo la kusini mwa Tanzania takribani miaka 100 iliyopita.

Na Mwandishi wetu:Masasi.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Damian Dallu amewataka Watanzania kujituma kufanya kazi ili wapate mahitaji yao ya lazima badala ya kutegemea misaada toka kwa matajiri.

Wito huo ameutoa wakati anaongoza Ibada ya Kumtawaza Padre Placidus Mtunguja kuwa Abate wa kwanza Mwananchi kuwaongoza Watawa wa Shirika la Mtakatifu Benedikto Ndanda, zilizofanyika Wilayani Masasi,mwanzoni mwa juma hili

Ametoa mfano, baada ya vita vya pili Wajerumani waliamua kufanya kazi kwa bidii na maarifa kiasi kwamba leo hii Taifa hilo  ni miongoni mwa Mataifa makubwa duniani yaliyo juu kiuchumi,na hivyo kuwahimiza Watanzania kuiga mfano huo badala ya kuwa Taifa tegemezi hata baada ya kufikisha miaka 50 tangu tupate Uhuru.

Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Kanisa,haoni mantiki ya baadhi ya wanasiasa wanaotafuta kuchaguliwa kwa kuwaahidi Watanzania kuwapatia huduma bure,kama za afya,elimu na maji;badala ya kuwahimiza wafanye kazi ili kujiinua kiuchumi.

 Abate wa kwanza mwananchi Padre Plasidus Mtunguja (mwenye fimbo katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na maaskofu mbalimbali wa kanisa katoliki kutoka nchini na mataifa ya nje mara baada ya abate huyo kutawazwa.

 BAADHI ya mapadre waliohudhuriwa ibada hiyo ya kutawazwa Padre Plasidus Mtunguja kuwa abate wa kwanza mwananchi.
KANISA katoliki parokia ya Ndanda,jimbo la Mtwara.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top