Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

OMARI MAKOTA AJITOSA RASMI KINYANG'ANYIRO CHA UBUNGE JIMBO LA RUANGWA KUPITIA CUF

TANGAZO
Na Mwandishi wetu,Ruangwa.
Maelfu ya wananchi  Wilayani Ruangwa wamejitokeza  kwa wingi kumsindikiza Mgombea Ubunge kupitia Chama cha Wananchi (CUF)  jimboni humo  Omari Makota alipokwenda kuchukua fomu ya Ubunge.

Msafara huo ulioanzia ofisi za CUF wilayani Ruangwa ulizunguka mji wote huku kukiwa na Matarumbeta,Mavuvuzela, ngoma, magari 30,matrekta matatu pamoja na  umati mkubwa wa watembea kwa miguu huku   Jeshi la Polisi likiimarisha ulinzi.
 
Tukio hilo la aina yake kuwahi kutokea katika medani za siasa wilayani humo limetokea juzi majira ya saa 8:30 alasili wakati mgombea huyo anayeonekana kuwa na mvuto kwa wananchi wengi wilayani Ruangwa alipowasili kwenye viwanja vya ofisi za msimamizi wa uchaguzi.

Mara baada ya kukabidhiwa fomu hiyo kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi jimbo la Ruangwa Nicholas Kombe, Makota aliyeambatana na mwenyekiti wa CUF wilayani Ruangwa Omari Likiwila aliwaomba wakazi wa Jimbo la Ruangwa kumuunga Mkono katika harakati zake za kugombea ubunge .

Alisema anatambua kuwa wananchi wana kiu ya mabadiliko  na kiu hiyo itaondolewa na yeye huku akijinasibu kuwa  anao uwezo wa kuleta mabadiliko ya kimaendeleo wilayani  Ruangwa kwani anatambua fursa mbalimbali zilizopo wilayani humo ambazo kwa sasa hazitumiki.

Kwa mujibu wa Makota alisema anazifahamu  njia sahihi za kufika kwenye kilele cha  mafanikio  na kwamba kwa muda wa miaka 16 aliyokuwa mtumishi wa umma amejifunza mengi kubwa likiwa ni namna ya kupata maendeleo ya wananchi.

“Wilaya ya Ruangwa ni miongoni mwa wilaya zenye Rasilimali nyingi kama vile madini,ardhi yenye Rutuba,Misitu…  lakini imekosa viongozi wa kuzisimamia fursa hizo  na endapo mtanipa nafasi ya kuwatumikia nitahakikisha fursa hizo zinatumika kwa manufaa ya Umma”. alisema Makota.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha Wananchi CUF Wilaya ya Ruangwa  Omari Liwikila alisema jimbo la Ruangwa kwa kipindi cha  takribani miaka 15 limekosa mwakilishi makini mwenye kuwatetea wakulima hasa katika suala zima la soko na bei nzuri ya mazao yao.

“Tangia mwaka 2005 zao la Korosho limekosa bei nzuri badala yake gharama za uendeshaji wa zao hilo zimekuwa kubwa ukilinganisha na bei ndogo ya shilingi 1000 ya Korosho inavyouzwa.

Akizungummzia kuhusu  zao la ufuta alisema mwaka 2013 kulikuwa na matumaini makubwa kwa wakulima wa zao hilo wilayani humo baada ya zao hilo kuuzwa kwa kilogramu moja shilingi   2000 hadi 2500.

Alisema kutokana na usimamizi mbovu wa viongozi waliopewa dhamana na wananchi  kwa sasa matumaini yameanza kutoweka kuanzia msimu wa mwaka 2014 /2015 baada ya zao hilo kuuzwa kwa bei ya shilingi  1800 hadi 1500 kwa kwa kilogramu moja.

“Wananchi wilayani Ruangwa huu ni mwaka wa mabadiliko…nawaomba tuchague viongozi ambao watakuwa watetezi kwa kusimamia maslahi ya umma”.alisema Liwikila.

Mwisho.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top