Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

NI RASMI....KUNDAMBANDA ACHUKUA FOMU YA UBUNGE KUPITIA CUF JIMBO LA MASASI.

TANGAZO
Na Mwandishi Wetu,Masasi.
MGOMBEA ubunge kupitia tiketi ya Chama cha wananchi CUF katika jimbo la Masasi mjini Ismail Makombe maarufu kwa jina la Kundambanda amechukua rasmi fomu ya kugombea jimbo hilo jana wilayani Masasi tayari kwa kuanza kuomba ridhaa kwa wananchi ili ateuliwe kuwa mbunge wa jimbo hilo.

Hatua ya Chama hicho kumsimamisha mgombea huyo kugombea kiti cha ubunge katika jimbo la Masasi mjini huenda kukaongeza mvutano uliopo ndani ya umoja wa Ukawa wilayani Masasi kwa kuwa maamuzi ya Chama hicho yanakinzana na makubaliano ya umoja huo katika vikao vyao vinavyoendelea kufanyika mjini hapa.

Makombe aliwasili jana majira ya saa 8:30 katika ofisi za NEC Halmashauri ya mji wa Masasi akiongozana na uongozi wa wilaya wa Chama hicho akiwemo mwenyekiti,Yusufu Matola na katibu Hassan Chaliche ili kuchukua fomu kwa ajili ya kuomba ridhaa ya kuchaguliwa kugombea ubunge kwenye jimbo hilo.

Katika siku za hivi karibuni katibu wa Chama hicho,Hassan Chaliche aliweka wazi kuwa hata kama Ukawa wilayani humo utaamua kumsimamisha mgombea mwingine kwenye jimbo hilo CUF haitakubaliana na maamuzi hayo na kwamba itachukua hatua ya kumsimamisha kundambanda kwa sababu ndiye mgombea anayekubalika na wananchi wa jimbo la Masasi.

Habari za uhakika kutoka ndani ya umoja wa Ukawa Masasi zinasema kuwa CUF wamekuwa na mabishano makubwa na vyama vya Chadema,NCCR mageuzi na NLD kuhusu utaratibu wa kumsimamisha mgombea katika jimbo la Masasi mjini na kueleza kuwa mgombea wao kundambanda amekuwa akihujumiwa kwa madai ya kigezo cha elimu aliyonayo.

Mvutano uliyopo ndani ya Ukawa wilayani Masasi unatokana na taarifa kuwa majimbo ya Masasi mjini,Ndanda na Lulindi yamekabidhiwa kwa Chama cha NLD ambapo Dkt, Emanuel Makaidi atasimama kuomba ridhaa katika jimbo la Masasi huku jimbo la Lulindi atasimama mke wa Makaidi na Ndanda ni Dkt.Mpelumbe  taarifa ambazo zimeanza kuzua balaa ndani ya umoja huo wilayani  Masasi.

Aidha kundambanda alipoombwa kuzungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu juu ridhaa yake ya kuomba kuteuliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo katibu wake chama cha CUF Hassan  Chaliche alimkataza asizungumze chochote na waandishi wa habari kwa sasa.


“Msheshimiwa kundambanda usizungumze chochote kama fomu umeshachukua tayari ingia ndani ya gari twende tukafanye mambo mengine waandishi nawaombeni mtuache twende,”alisema Chaliche huku akifunga mlango wa gari kwa jazba. 
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top