Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO

MAELFU YA WAOMBOLEZAJI WAMZIKA ALIYEKUWA MBUNGE WA VITI MAALUMU KUPITIA CHAMA CHA WANANCHI CUF MKOA WA MTWARA.
Marehemu Clara Daniel Mwatuka alizaliwa Mei 11, 1946 huko katika kijiji cha Miyuyu Wilaya ya Newala mkoani Mtwara.

Alipata elimu ya Msingi katika shule ya msingi Newala  kati ya mwaka 1953-1956.Mwaka 1957-1960 aliendelea na masomo katika shule ya msingi ya wasichana ya mtakatifu Maria huko huko wilayani Newala.
Marehemu alijiunga na elimu ya sekondari  mwaka 1976 na kufanikiwa kuhitimu  mwaka 1979 huko katika shule ya sekondari Mbinga  mkoani Ruvuma.

Mwaka 1989-1990 alisoma masomo ya sekondari katika shule ya sekondari ya Kitangari iliyopo wilayani Newala na mwaka 1991-1992 alisoma katika chuo cha ualimu Mtwara na kufanikiwa kupata ualimu daraja la III A.
 Jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu mbunge wa viti maalumu kupitia chama cha wananchi CUF mkoa wa Mtwara Clara Daniel Mwatuka.

 JENEZA lililokuwa na mwili wa marehemu mbunge wa viti maalumu mkoa wa Mtwara kupitia CUF Clara Mwatuka likishushwa kaburini.

Mwaka 1979 -1993 marehemu Clara Mwatuka aliajiriwa kama mwalimu katika Halmashauri ya wilaya ya Masasi mkoani Mtwara na alifanya kazi ya ualimu katika shule mbalimbali za msingi ikiwemo Ndanda na Nanganga wilayani masasi.
 KISIASA
Marehemu alikuwa mwanachama wa chama cha wananchi CUF kati ya mwaka 1993-2010 na kwamba katika kipindi hiko aliwahi kuwa mkurugenzi wa idara ya  uchaguzi kupitia chama chake wilayani Masasi.

 NAIBU spika wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Job Ndugai wakati akitoa salamu za Bunge kwenye mazishi ya marehemu Clara mwatuka mbunge wa viti maalumu CUF mkoa wa Mtwara hii leo kijijini Nanganga wilayani Masasi.
MKUU wa wilaya ya Masasi Bernald Nduta akizungumza wakati wa mazishi ya aliyekuwa mbunge wa viti maalumu mkoa wa Mtwara kupitia chama cha wananchi CUF.

Mwaka 1997-2010 alikuwa mjumbe wa Halmashauri kuu ya CUF ambapo mwaka 2010-2015 aliteuliwa kuwa mbunge wa viti maalumu kupitia chama cha wananchi CUF mkoa wa Mtwara.
Akiwa bungeni amewahi kuwa mjumbe kwenye kamati ya kudumu ya miundombinu.
Marehemu alifariki Agosti 9, 2015 kwa ajali ya gari huko katika milima ya Miyuyu wilayani Newala.
Marehemu ameacha Mume,watoto na wajukuu.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top