Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI YAZINDUA RASMI BODI YA HUDUMA ZA AFYA

TANGAZO
Na Clarence Chilumba,Masasi.
HALMASHAURI ya wilaya ya Masasi mkoani Mtwara imezindua rasmi bodi ya huduma za Afya za Halmashauri lengo likiwa ni kugatua madaraka kutoka serikali kuu hadi kwa wananachi ambao ndio waathirika wakubwa wa masuala ya afya ikiwemo vifo vya watoto pamoja na akinamama wakati wa kujifungua.
Akizungumza jana wakati wa uzinduzi huo  mkuu wa wilaya ya Masasi Bernald Nduta alisema changamoto kubwa inayoikabili sekta ya afya nchini ni ukosefu wa dawa na vifaa tiba na kwamba ni vyema sasa serikali kupitia wizara ya afya na ustawi wa jamii ikatenga fedha za kutosha ili kuweza kukabiliana na changamoto hizo kupitia bodi hiyo ya afya wilayani humo.
Uzinduzi wa bodi hiyo ulifanyika jana kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo na kuhudhuriwa na wakuu wa idara na vitengo,wajumbe wote wa bodi hiyo wakiwemo wa kuchaguliwa (wanaopiga kura),wawakilishi wa watumiaji huduma za afya kutoka kwenye jamii, makundi yanayotoa huduma,mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii anayewakilisha madiwani pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo akiwemo mganga mkuu na ofisa mipango.
Alisema watumishi wa afya pia wanapaswa kufanya kazi kwa kufuata maadili na kanuni za utumishi wa umma huku akionya kuwa mtumishi wa idara ya afya atakayebainika kuenenda kinyume na utaratibu atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kumsimamisha kazi.
Alisema kwa sasa watumishi wa idara ya afya nchini wamekosa uzalendo mazingira yanayopelekea kuwapo kwa malalamiko mengi kwenye Hospitali,vituo vya afya na zahanati za serikali ambapo aliiasa bodi hiyo kufuatilia mara kwa mara utendaji kazi wa watumishi wa idaara hiyo mara kwa mara.
Kwa mujibu wa mkuu huyo wa wilaya ya Masasi alitoa agizo kwa ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Masasi Beatrice Dominick kuhakikisha kuwa wanaandaa mafunzo haraka iwezekanavyo kwa ajili ya wajumbe wa bodi hiyo ili waweze kufanya kazi wakijua majukumu yao pamoja na mipaka yao kwa lengo la kuepusha migongano isiyo ya lazima.
Kwa upande wake mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Masasi Dkt.Jerry Kanga alisema uundaji wa bodi za huduma za afya za halmashauri na kamati za vituo ni utekelezaji wa mabadiliko katika sekta ya afya na serikali za mitaa na kwamba uhalali wa kuwepo kwa bodi hiyo unatokana na sheria ya serikali za mitaa (mamlaka za wilaya) sura namba 287.
Alisema moja ya jukumu kubwa la bodi hiyo ni kuhakikisha jamii inapata huduma bora za afya inazozimudu,inazozimudu pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa rasilimali na mgawanyo wake kwa kuzingatia mahitaji katika ngazi zote za huduma na matumizi bora.
Kwa mujibu wa Dkt.Kanga alisema pia bodi inawajibu wa kufanya kazi kwa karibu na Halmashauri ya wilaya pamoja na jamii kwa ujumla ambapo pia inapaswa kupokea taarifa na kupitia taarifa za utekelezaji wa mipango ya afya ya halmashauri toka kwa timu ya uendeshaji wa huduma za afya za halmashauri.
Mwisho.

WAJUMBE wa Bodi ya Huduma za Afya za Halmashauri ya wilaya ya Masasi wakifuatilia hotuba ya mkuu wa wilaya ya Masasi Bernald Nduta jana wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top