Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

POLISI WA KIKE NCHINI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA UADILIFU ILI KUONDOA MALALAMIKO

TANGAZO
Kamanda wa polisi mkoa wa Lindi Renatha Mzinga

Na Clarence Chilumba,Masasi.
KAMANDA wa polisi mkoa wa Lindi Renatha Mzinga amewataka askari wa kike nchini wahakikishe wanatimiza majukumu yao kikamilifu ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa weledi na nidhamu katika  kitengo cha dawati la jinsia chenye waathirika wengi wa matukio ya unyanyasaji nchini.
 Wito huo ameutoa leo wilayani Masasi wakati wa uzinduzi wa mtandao wa polisi wanawake Tanzania (TPF-NET) pamoja na dawati la jinsia  ambapo alisema mtandao huo ni chombo pekee cha ukombozi kwa askari wa kike ambao kwa kipindi kirefu sasa wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na unyanyasaji kutoka kwa baadhi wa askari wa kiume.
Alisema TPF-NET iliundwa kwa lengo la kupambana na vitendo vyote vya unyanyasaji wanavyovipata askari wa kike kutoka kwa raia pamoja na baadhi ya askari wa kiume na kwamba uwepo wa mtandao huo ambao kwa sasa umeenea kila kituo cha polisi nchini umesaidia kuondoa changamoto hizo.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Lindi alisema licha ya kutetea haki za askari wa kike TPF-NET pia husimamia nidhamu pamoja na maadili kwa wanachama wake wote ambao ni askari wote wa kike wa jeshi hilo.
“Ndugu zangu askari wa kike leo tunafanya uzinduzi wa mtandao huu…mtambue kwamba chombo hiki ni muhimu kwetu kwa maslahi yetu hivyo kila alipo askari wa kike nchni anapaswa kutimiza majukumu yake kwa kufuata kanuni na sheria za jeshi la polisi Tanzania”.alisema Mzinga.
Alisema askari wa kike wanapaswa kutumia fursa mbalimbali zilizopo kwenye jeshi hilo ikiwemo elimu kwa kujiendeleza ili nao waweze kufikia nafasi za juu za uongozi wa jeshi la polisi kama wao walivyoweza ambao kwa sasa wako kwenye nafasi za juu za uongozi.
Awali akisoma risala fupi mmoja wa wanachama wa mtandao huo Pendo Pakacha alisema wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali katika uetekelezaji wao wa majukumu ya kila siku ikiwemo ukosefu wa nyenzo za kutendea kazi, ukosefu wa rasilimali fedha pamoja na ofisi ya mtandao kwani kwa sasa mtandao hauna ofisi.
Alizitaja changamoto zingine kuwa ni ukosefu wa mtaji wa kuanzisha mradi hivyo kushindwa kufikia moja ya malengo ya mtandao huo ya kuinua vipato vya askari wa kike ambapo walimuomba kamanda wa polisi mkoa wa Lindi kuwafikishia kilio chao kwa uongozi wa juu wa jeshi hilo nchini.
Mtandao wa polisi wanawake Tanzania (TPF-NET) ulianzishwa rasmi wilayani Masasi mwaka 2009 ambapo kwa sasa una jumla ya wanachama 41.

 KAMANDA wa polisi mkoa wa Lindi Renatha Mzinga akiwa na Afisa Mnadhimu wa jeshi la polisi  mkoa wa Mtwara George Salala wakipiga makofi  wakati wakipokea maandamano ya askari wa kike wa wilaya ya Masasi hii leo wakati wa uzinduzi wa Mtandao wa polisi wa kike wilayani humo.
 BAADHI ya askari wa kike wa jeshi la polisi wilaya ya Masasi wakiwasili kwenye ukumbi wa miduleni mara baada ya kumaliza kwa maandamano yao yaliyoanzia viwanja vya polisi Masasi na kupita kwenye Barabara kuu iendayo Mkoani Mtwara na hatimaye kwenye Barabara ya Mkapa.
 Askari wa kike ambao ni wanachama wa Mtandao wa Polisi wa kike Tanzania (TPF-NET) wilaya ya Masasi wakiwa kwenye ukumbi wa Miduleni wilayani Masasi wakati wa uzinduzi wa Mtandao wao hii leo.
 MAANDAMANO ya askari wa kike wa jeshi la polisi wilaya ya Masasi yakipita kwenye Barabara ya Mkapa hii leo wakiwa na wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Masasi pamoja na wanafunzi wa sekondari ya kutwa ya Masasi.
 ASKARI wa kike wa wilaya ya Masasi pamoja na wanafunzi wa sekondari ya wasichana Masasi wakimsikiliza kwa makini mgeni rasmi ambaye ni kamanda wa polisi mkoa wa Lindi Renatha Mzinga wakati wa uzinduzi wa TPF-NET.

MAANDAMANO ya askari wa kike wa jeshi la polisi wilaya ya Masasi  yakiwasili kwenye ukumbi wa Miduleni wilayani Masasi hii leo.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top