Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

NALIENDELE WAGUNDUA MBEGU BORA CHOTARA YA ZAO LA KOROSHO KWA MSIMU WA 2014/2015.

TANGAZO
Na Haika Kimaro,Mtwara.
TAASISI ya utafiti wa kilimo Naliendele iliyopo mkoani Mtwara imefanikiwa kugundua mbegu bora chotara 24 za zao la korosho kwa mwaka wa fedha 2014/2015 na kuifanya taasisi hiyo kuwa ya kwanza barani afrika kwa ugunduzi wa idadi kubwa ya mbegu za zao hilo.
Hayo yameelezwa na mtafiti kiongozi wa zao la korosho nchini Dkt. Peter Massawe alipokuwa akiongea na wajumbe wa mkutano wa mapitio ya shughuli za utafiti wa zao hilo na kuwa tayari mbegu hizo zilisajiliwa mapema Februari mwaka huu zikiwa na sifa za ukinzani wa magonjwa na wadudu waharibifu kutoa mavuno mengi na ukubwa wa korosho hizo.
“Utafiti wa korosho umefanikiwa kutoa mbegu chotara 24 ambazo zilisajiliwa Februari mwaka huu na hii imeifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika na kama sio duniani katika kutoa mbegu chotara iliyopitia katika mfumo wa utafiti ya kuweza kufanya majaribio katika mazingira matatu tofauti na kutumia data hizo na imeweka rekodi za kidunia,’alisema Massawe na kuongeza
“Na kwa upande wa Tanzania wizara ya kilimo idadi ya mbegu za kilimo walizokusudia kutoa imepanda kutokana na mchango unaotoka katika mbegu hizi 24 za zao la korosho,”alisema.
Akizungumza kaimu mkurugenzi wa taasisi hiyo Dkt. Omary  Mponda alisema  mafanikio hayo ni ya kujivunia kwa taasisi yake na wadau wa zao la korosho nchini na wakulima sasa kuanza kutumia mbegu hizo.
“Kubwa zaidi ni kwamba baada ya ugunduzi wa mbegu hizi wakulima ama maafisa ugani wakishafahamu wakatengeneze vitalu ili ikapandwe na uweze kusambazwa kwa wakulima walio wengi na mategemeo yetu ni kuwa mbegu hizi zitachangia uzalishaji kwa wingi hapa nchini,”alisema Dkt. Mponda
Akizungumza Afisa ugani toka Mkuranga mkoa wa Pwani Julitha Bulali alisema  mkutano  kikao hicho kimewawezesha kupata taarifa mpya za kiutafiti na hivyo kuwawezesha kuwapelekea wakulima taarifa nzuri na zilizo sahihi.
Kwa mujibu wa bodi ya korosho Tanzania uzalishaji wa zao hilo umeongezeka kufikia tani laki moja tisini na sita elfu katika msimu uliopita huku matumizi ya mbegu bora na teknolojia sahihi za uzalishaji wa zao hilo zikielezwa kuwa na mchango kubwa katika kukuza kiwango cha uzalishaji na ubora wa korosho nchini.
Mwisho.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top