Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MURJI ASHINDA KESI YA MADAI,MAHAKAMA YAAMURU ALIPWE MILIONI 51.5-NCCR MAGEUZI WADAI NI UONEVU....

TANGAZO
Mbunge wa Mtwara Mjini Asnain Murji.
Na Haika Kimaro,Mtwara.
Mahakama kuu kanda ya Mtwara imemtaka Mwenyekiti wa chama cha NCCR-MAGEUZI wilaya ya Mtwara mjini, Ulledi Abdalla kumlipa mbunge wa Mtwara Mjini,Hasnei Murji (CCM) pesa kiasi cha 51.5 milioni kama gharama za kuendeshea kesi.
Hatua hiyo imekuja baada ya Mbunge Murji  kushinda katika katika kesi ya madai ikiwa ni baada ya kushinda katika kesi ya pingamizi la uongozi katika nafasi ya ubunge iliyokuwa imefunguliwa na Ulledi baada ya Murji kutangazwa kama Mbunge katika jimbo hilo.
Awali katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 Ulledi alikuwa akiwania jimbo hilo la Mtwara mjini kupitia chama cha CUF ambapo hakuridhishwa na matokeo na kuamua kufungua kesi.
Akisoma shauri hilo mahakamani hapo ,Naibu msajili wa mahakama kuu Mtwara, Hussen Mushi alisema  ni wajibu wake kusoma maamuzi kwa niaba ya msajili aliyekuwepo awali na ndipo aliposema Ulledi anatakiwa kulipa gharama hizo na kama hajaridhika na maamuzi hayo anaruhusiwa kuandaa reference judgement.
Awali mahakamani hapo Ulledi aliyewakilishwa na katibu wake binafsi, Fatuma Sinani ambaye pia ni mjumbe wa halmashauri kuu  ya taifa aliieleza mahakama kuwa Ulledi kwa sasa yuko katika  chuo  cha kiislamu cha Morogoro na kwamba barua ya kumtaka awepo mahakamani hapo aliipata juzi mchana wakati tayari alikuwa ameshajiandaa kwa ajili ya kurudi chuo kufanya mitihani.
Hata hivyo baada ya kutoka mahakamani katibu huyo aliwaeleza waandishi wa habari kuwa mahakama haikutenda haki na kwamba wataendelea kukata rufaa.
“ Judgment nimeipokea tutakata rufaa haki haijatendeka kwani sisi kesi tuliyoileta ni nyingine lakini imepindishwa,”alisema Sinani
Akizungumza Hussein Mtembwa wakili wa kijitegemea aliyekuwa akimwakilisha wakili Peter Kibatala kwa niaba ya Murji mahakamani hapo aliwaambia wanahabari  kuwa hiyo ilikuwa ni hukumu ndogo ya madai na mahakama iliona madai yao ni ya msingi ndipo ilipotoa maamuzi ya kulipwa kwa kiasi hicho cha pesa.
“Ilikuwa ni hukumu ndogo ya madai na mahakama iliona madai yetu ni ya msingi na hukumu ndio imetolewa anatakiwa kulipwa Sh 51.5 milioni , na kama wataona kuna haja ya kuandaa reference ni haki yao cha msingi ni kufuata sheria na taratibu,”alisema wakili Mtembwa.
Alipotafutwa mbunge huyo alisema kuwa mahakama ndio sehemu ya mwisho ambapo haki hupatikana na kusema kuwa yote hayo yametokana na pingamizi la ushindi wa ubunge katika jimbo analoongoza sasa na kudai kuwa mpinzani wake huyo alikata rufaa hadi kufikia mahakama ya rufaa lakini bado mahakama imeona ana haki ya kulipwa.
Mwisho.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top