Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

WEZI WAVUNJA KANISA WAFANIKIWA KUIBA CHOMBO CHA KUHIFADHIA EKARISTI TAKATIFU (TARBENACULO)

TANGAZO
Tarbenaculo liko nyuma ya Pazia kwenye maandishi mekundu
Na Clarence Chilumba,Ruangwa.
Watu watano wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamevamia na kuvunja madirisha katika kanisa katoliki la matakatifu Joseph Mfanyakazi parokia ya Malolo jimbo la Lindi na kufanikiwa kuiba kifaa kinachotumika kuhifadhia ekaristi takatifu (TABERNACULO) kwa madai kuwa kifaa hicho kimetengenezwa kwa kutumia dhahabu.
Tukio hilo la kushangaza ambalo limewaacha waumini wa kanisa hilo wasijue cha kufanya limetokea Alhamisi  April 16 mwaka huu majira ya saa 8:30 usiku  ambapo watu hao walivamia na kuvunja baadhi ya madirisha ya kanisa hilo lenye historia kubwa nchini lililojengwa mwaka 1939.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo paroko wa kanisa katoliki parokia ya Malolo,Theophan Membe alisema siku ya tukio hakuwepo kanisani hapo na kwamba alikuwa safarini jimboni Lindi kuhudhuria misa takatifu ya mapadre wa jimbo la Lindi  iliyoongozwa na Askofu wa jimbo hilo Mhashamu Bruno Ngonyani.
Alisema alirejea parokiani hapo siku ya ijumaa ambapo wakati anasalimiana na mpishi wake alimpa taarifa hizo kuwa kanisa limevunjwa madirisha na watu wasiofahamika na Tarbenaculo limeibiwa na kwamba hawajui ni nani amehusika na tukio hilo ambalo amekiri tangu aanze kufanya kazi ya upadre hajawahi kusikia hata kuona kifaa hicho kikiibiwa.
“Tukio hili limenisikitisha sana kwani tangia nianze kufanya kazi hii ya upadre haijawahi kutokea… huu ni ujinga kwa waliohusika na wizi huo kwani najua wanadhani kuwa kifaa kile kimetengenezwa kwa dhahabu nasikitika sana kizazi hiki cha Dijitali kuwa na mawazo ya kijinga namna hii…kama mungu anasikia kilio change naomba watu hawa walaaniwe”.alisema Membe kwa uchungu.
Alisema baada ya kushuhudia kuwa ni kweli alimpa taarifa mwenyekiti wa kigango cha Malolo Cleophas Nnonjela kuhusu tukio hilo na kwamba siku ya jumamosi walitoa taarifa kituo cha polisi Ruangwa kilichomtaka mwenyekiti huyo kwenda na katekista wa kigango hicho Moris Nguli.
Kwa mujibu wa Padre huyo alisema parokia ya Malolo ni miongoni mwa parokia zilizotoa wasomi wengi mkoani Lindi kutokana na historia yake ya kuingia mapema kwa wamisionari waliongia kijijini hapo mwanzoni mwa miaka 1890 na kufanikiwa kujenga shule ambayo imetoa maprofesa akiwemo profesa Max Mmuya,marehemu Dkt.David Mwambe na viongozi kadhaa waliowahi kushika nyadhifa mbalimbali nchini.
Alisema kwa kwa mujibu wa sheria za Roma za kanisa hilo mahali ambapo Tarbenaculo huibiwa ukristo hufa kwa muda mpaka pale wahusika hao walioiba kifaa hicho watakapokiri kuwa ni kweli wameiba mbele ya waumini wa kanisa hilo ndipo askofu wa jimbo hilo atakapoondoa dhambi hiyo ya mauti kutoka kwa waumini kwenda kwa wezi hao ambao amekiri kuwa ni dhahiri adhabu ya moto inawasubiri.
Huduma ambazo hazitakuwepo kwa sasa kwa waumini wa kigango hicho ni pamoja na ibada ya jumapili,misa ya kila siku asubuhi,misa ya katekista,upigwaji wa kengele zinazoashiria masaa kwa waumini hao ikwemo majira ya saa 12:00 asubuhi,saa sita mchana na saa 12:00 jioni pia nazo hazitakuwepo.
Alisema katika kipindi hicho pia huduma kama za ubatizo,kipaimara,komunio takatifu,kitubio,misa za mazishi,mpako kwa wagonjwa,sherehe za ndoa pamoja na masuala yote ya msingi yanayohusu kanisa katoliki huku akikiri kuwa waumini wa vigango vitatu vilivyobaki wataendelea kupata huduama hizo kama kawaida.
“Binafsi ninachosubiri kwa sasa ni muongozo kutoka kwa baba askofu juu ya hatima ya suala hili…jana nimeongea na makamu wa askofu baba Angelus Chitanda  ambaye alinitaka nisubiri mwongozo lakini kiimani ya dhehebu letu la katoliki hapa hakuna ukristo tena mapaka pale wezi watakapopatikana na kukiri mbele ya waumini kinyume na hapo ukristo unakufa mahali ambapo ni chimbuko la parokia ya Malolo”. Alisema Membe.
Katika hatua nyingine watu wasiofahamika walivamia na kufanikiwa kuvunja mlango wa nyumba anayoishi padre huyo parokiani hapo usiku wa jumapili ya wiki hiyo hiyo lilipotokea tukio la wizi wa Tarbenaculo ambapo hawakufanikiwa kuiba chochote kutokana na mpishi wa padre huyo ambaye alilala ndani ya nyumba hiyo kuamka na wezi hao kutokomea kusikojulikana.
“Sijui ni nini nimewakosea waumini wa kigango hiki cha Malolo…mpaka wanafikia kunifanyia vitendo vya kinyama kama hivi ambavyo haviendani na maadili ya dini ya kikristo nadhani hapa kuna ajenda ya siri waliyonayo watu hawa hivyo ni vyema waiweke wazi”.alisema Membe aliyeonekana kukerwa na vitendo hivyo.
 Kifaa ambacho hutumika katika kuhifadhi "EKARISTI TAKATIFU" ambacho kwa nje huonekana kama kimetenegenezwa kwa kutumia DHAHABU wakati si kweli mazingira ambayo vijana hudhani ni Dili.
 PAROKO wa kanisa katoliki parokia ya Malolo padre THEOPHANI MEMBE ambaye ameonesha kukerwa na kitendo kilichofanywa na Watu hao ambao mpaka sasa hawajulikani huku akiahidi kusitisha huduma ya ibada kwenye kigango hicho.
 KANISA Takatifu la Mtakatifu JOSEPH MFANYAKAZI Parokia ya Malolo Jimbo la Lindi katika mkoa wa Lindi ambamo TARBENACULO hilo limeibiwa na watu wasiofahamika usiku wa kuamkia April 17, 2015.KANISA hilo limejengwa mwaka 1939.

 NYUMBA anayoishi Paroko wa parokia ya Malolo Fr.Theophan Membe ambayo Mlango wake kwa huko nyuma umevunjwa na watu wasiofahamika waliokuwa na lengo la kuiba.
 ASKOFU wa Jimbo la Lindi Mhashamu BRUNO NGONYANI ambaye anasubiriwa kutangaza adhabu kwa waumini wa kanisa katoliki kigango cha Malolo wakati wowote kutoka sasa mpaka pale waliohusika watakapokiri mbele ya waumini.
 KIFAA hiko alichoshika PADRE Rangi yake hufanana na hiyo TARBENACULO ambacho vijana wengi wa kanisa hilo hudhani kuwa ni DHAHABU.


SHULE ya Msingi Malolo Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi ambayo iko jirani na kanisa lililoibiwa kifaa hicho cha kuhifadhia Ekaristi Takatifu.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top