Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MAFUNZO KWA WAANDISHI WA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU YAANZA RASMI MASASI.

TANGAZO
 Na Clarence Chilumba,Masasi.
Waandishi wasaidizi,wataalamu wa BVR KIT pamoja na wataalamu wa TEHAMA Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara wametakiwa kufanya kazi hiyo kwa weledi mkubwa ili kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza katika zoezi la uborshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura linalotarajia kuanza April 24,2015.
Rai hiyo imetolewa jana na kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Masasi Mzenga Twalibu wakati anafungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wasaidizi wa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.
Alisema suala kazi ya uboreshaji wa daftari hiyo ni nyeti hivyo wanapaswa kuzingania maadili katika utendaji wa kazi hiyo ili wananchi wapate fursa ya kushiriki kwenye uchaguzi mkuu ujao pamoja na zoezi la kuipigia kura ya ndiyo au hapana katiba inayopendekezwa.
Kwa mujibu wa Mzenga alisema ofisi ya mkurugenzi imewaamini na ndio maana wakapewa kazi hiyo kulingana na vigezo vilivyowekwa wakati wa kutangazwa kwa kazi hiyo nyeti kwa maslahi ya taifa kwa vizazi vya sasa na vile vijavyo.
“Mmeteuliwa kuwa miongoni mwa watakaofanya kazi hii muhimu kwa taifa…hatutegemei kuwa mmoja wenu atafanya ndivyo sivyo pale zoezi hili litakapoanza ambapo ukweli ni kwamba kwa Yule atakayeharibu kazi hii atachukuliwa hatua kali za kisheria na ndio maana kabla ya zoezi hili halijaanza ni lazima mle kiapo”.alisema Mzenga.
Alisema zoezi hilo linafuatiliwa kwa karibu na wadau mbalimbali nchini wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa,waangalizi wa ndani wa uchaguzi,mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na wadau wengine hivyo ni wajibu wao watekeleze majukumu yao kwa ufanisi mkubwa.
Mafunzo hayo ya siku mbili yameanza jana na yanatarajiwa kukamilika kseho ambapo jumla ya washiriki 210 watapatiwa mafunzo hayo yatakayowawezesha kuandikisha wananchi kwenye zoezi la uboreshajiwa daftari la kudumu la wapiga kura.
Mwisho.
 Ofisa Uchaguzi wa Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara SHAIBU MWAKATIKA(Kushoto) wakati anatoa maelekezo ya namna ya utumiaji wa mashine za BVR kwa maofisa uchaguzi wa ngazi ya Kata hii leo wakati wa mafunzo ya siku mbili kwenye ukumbi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Masasi.
Hakimu wa mahakama ya wilaya ya Masasi HALFANI ULAYA akiwaapisha waandikishaji wa zoezi la daftari la kudumu la wapiga kura kwenye ukumbi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Masasi.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top