Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

ALIYEKUWA RAIS WA MISRI MOHAMMED MOSRI ATUPWA JELA MIAKA 20

TANGAZO
Aliyekuwa Rais wa Misri Mohammed Mosri
Makahama nchini Misri imemuhukumu aliyekuwa rais wa zamani Mohammed Mosri kifungo cha miaka 20 gerezani kutokana na kuuawa kwa waamdamanaji wakati akiwa madarakani.
Hii ndiyo hukumu ya kwanza kutolewa kwa Morsi tangu aondolewe madarakani na jeshi la nchi hiyo mwaka 2013 kufuatia maandamano makubwa mitaani ya kupinga uongozi wake.
Yeye pamoja na viongozi wengine wa Muslim Brotherhood walilaumiwa kwa kuwachochea wafuasi wao kumuua mwandishi wa habari na waandamanaji wa upinzani wakati wa makabiliano nje ya ikulu ya rais mwishoni mwa mwaka 2012.
Wakati umati ulipokusanyika nje ya Ikulu, Morsi aliwaamrisha polisi kuwatawanya lakini wakakataa kufanya hivyo. Baadaye Muslim Brotherhood waliwaleta wafuasi wao ambapo watu 11 waliuawa kwenye makabiliano, wengi kutoka Muslim Brotherhood.
Kabla ya kutolewa hukumu ya leo, Muslim Brotherhood walimlaumu rais wa sasa Abdul Fatta al-Sisi kwa kutumia mahakama kama silaha kuhalalisha utawala wake kwa kumkandamiza Morsi. Mara baada ya hukumu hiyo, chama cha Muslim Brotherhood kimeitisha maandamano kote nchini humo hali iliyosababisha makabiliano makali na polisi.
Kwa mujibu wa mahakama hiyo, rufaa ya hukumu hiyo iko wazi na mshitakiwa anaweza kufanya hivyo. Mohammed Morsi ndiye rais wa kwanza katika Taifa hilo kuchaguliwa kwa njia ya kidemokrasia baada ya kuangushwa utawala wa muda mrefu wa Hosni Mubarak na waandamanaji, lakini ulidumu kwa mwaka mmoja tu kabla ya kuangushwa na jeshi.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top