Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YATHIBITISHA CHAMA CHA ACT- TANZANIA KUITWA ACT-WAZALENDO..

TANGAZO

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini imekubali maombi ya chama hicho huku ikiwataka kurudisha cheti cha usajili wa awali na kupewa cheti kingine.

Awali ACT-Wazalendo ilipata usajili kwa jina la ACT-Tanzania na baadae kuomba kulibadili jina hilo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, ameridhika na maelezo yaliyokuwa yametolewa na uongozi wa chama hicho wa sababu za kuamua kubadili jina la chama hicho kutoka ACT-Tanzania hadi ACT-Wazalendo.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwa vyombo vya habari jana jiijini Dar es Salaam, Jaji Mutungi alijibu ombi hilo kwa njia ya barua.

Katika taarifa hiyo inaeleza: "Nikurejeshe kwenye barua yenye kumbukumbua namba AC-HQ/MSJ/2015 ya Aprili 15, mwaka 2015 ikisomwa sambamba na barua yangu yenye kumbukumbu namba HA.322/362/20/80 ya Aprili 13, mwaka 2015 kuhusu suala tajwa hapo juu".

Jaji Mutungi alieleza kuwa, alisoma na kuyatafakari kwa kina maelezo katika barua ya ACT-Wazalendo, na kwamba ameridhika na maelezo yao kuhusu jina jipya la chama hicho kwa mujibu wa kanuni ya 7 ya kanuni za usajili wa vyama vya siasa.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top