Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

DK.MAGUFULI,NIOMBEENI NIWEZE KUTIMIZA AHADI NILIZOZITOA KWA WATANZANIA WAKATI WA KAMPENI

TANGAZO


RAIS Dk John Magufuli amewataka Watanzania wa dini zote na viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali, kuendelea kumuombea ili atekeleze ahadi alizozitoa pamoja na kuinua maisha ya Watanzania.

Dk Magufuli aliyasema hayo kwenye Ibada ya Mavuno iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam jana. Aliwashukuru pia wananchi wote waliomuombea na kufanikisha kuchaguliwa kuwa Rais wa Tanzania wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Katika siku ya nne akiwa ofisini na Jumapili yake ya kwanza tangu alivyoapishwa kuwa Rais wa Tanzania, aliwasili kanisani hapo saa 12.50 asubuhi akiambatana na mkewe, Janet. “Natoa shukurani kwa Watanzania wote wenye imani za kidini tofauti kwa sala zao.

Nawaomba waendelee kuniombea ili niweze kutekeleza ahadi nilizotoa, lakini pia niinue maisha ya Watanzania,” alisema Dk Magufuli alipopewa nafasi ya kuzungumza. Alisema anaamini kuwa ana deni kubwa kwa Watanzania hivyo aliahidi kufanya kazi kwa bidii na kuboresha utoaji wa huduma kama njia ya kutimiza wajibu wake kwao.

“Sala zenu ni muhimu sana, zitaniwezesha kufikisha nchi yetu katika hatua nyingine bora zaidi,” alisisitiza. Awali, wakati akimkaribisha kanisani hapo, Mwenyekiti wa Parokia ya Mtakatifu Petro, Dk Adelhelm Meru, alisema kwa kawaida Watanzania na Waafrika kwa ujumla wana utamaduni wa kutoa shukurani pale wanapopata mafanikio.

Huu ni utamaduni tuliorithi tangu vizazi na vizazi ndio maana nakuomba leo mheshimiwa Rais, uje usalimie katika mkutano huu,” alisema Dk Meru ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii. Dk Magufuli ni mmoja wa waumini katika parokia hiyo ya Mtakatifu Petro kama ilivyokuwa kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top