Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MAKAMPUNI YA UWEKEZAJI KANDA YA KUSINI YATAKIWA KUHIFADHI MAZINGIRA

TANGAZO
Na John Kasembe,Mtwara.
Makampuniya uwekezaji yaliyoonesha nia ya kuwekeza katika uvunaji wa rasilimali zinazopatikana katika mikoa ya kusini ya Lindi, Mtwara pamoja na  Ruvuma yametakiwa kuhakikisha yanazingatia uhifadhi wa mazingira ili kuepusha neema ya uwekezaji huo kugeuka balaa kwa ustawi wa mazingira.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Saidi Mwambungu ametoa wito huo jana wakati wa ufunguzi wa jukwaa la maendeleo endelevu kwa mikoa ya kusini yaliyoandaliwa na shirika la kimataifa la uhifadhi wa misitu (WWF) yaliyofanyika kwenyeukumbi wa NAF Beach mjini Mtwara.

Alisema makampuni mengi yameonesha nia ya kuwekeza katika mikoa ya kusini katika uvunaji wa rasilimali ya gesi, mafuta, madini, uranium na makaa ya mawe na kwamba uwekezaji huo ni lazima uzingatie uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake mratibu wa uhifadhi wa ardhi wa  WWF Profesa Husein Sosovele alibainisha kuwa hakuna maendeleo endelevu yanayopatikana bila ya kuhifadhi mazingira ya maeneo husika,ambapo ameeleza kuwa bado mazingira ya mikoa ya kusini hayajaharibiwa kutokana na uwekezaji uliopo.

Mwisho.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top