Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

WANANCHI MASASI WAPONGEZA HOTUBA YA DK.JOHN MAGUFULI,WENGI WAMFANANISHA NA NABII MUSA.

TANGAZO
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli.

Na Clarence Chilumba,Masasi.
Wananchi wilayani Masasi mkoani Mtwara wameimwagia sifa hotuba iliyotolewa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli wakidai imesheheni matumaini mapya kwa watanzania wa kipato cha chini.

Hotuba hiyo ameitoa hii leo bungeni mjini Dodoma ikiwa ni hotuba yake ya kwanza ambayo ni rasmi kuitoa tangu aapishwe kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Novemba 5 mwaka huu.

Wakizumgumza na blog ya mtazamo mpya hii leo mara baada ya hotuba hiyo kumalizika wananchi hao walisema wana imani kubwa na Rais Magufuli kwa kuwa ameonesha wazi kuwa anayo dhamira ya dhati kutoka moyoni mwake ya kuwakomboa watanzania.

Kassian Ashapira mkazi wa mji wa Masasi alisema hotuba ya Rais Magufuli imeonesha ni kwa namna gani serikali yake ya awamu ya tano itakuwa na kwamba cha msingi kwa sasa ni kwa viongozi wa vyama vya siasa na wananchi kwa ujumla kumuunga mkono.

Alisema wao kama wananchi wa kawaida wamepokea kwa mikono miwili uamuzi wake wa kufuta safari za viongozi nje ya nchi,matumizi ya magari yenye thamani kubwa pamoja na matibabu ya nje kwa viongozi wa serikali yanayopoteza fedha nyingi za serikali.

Kwa mujibu wa Ashapira alisema watanzania kwa sasa wanahitaji kuona viongozi wa kitaifa wakiwa kama Dk.Magufuli ambaye ameonesha wazi kuwa ahadi alizozitoa wakati anaomba ridhaa kwa watanzania ya kuwa Rais zitatekelezwa kwa kiwango kikubwa na kwamba serikali hii ni ya neema kwao.

Kwa upande wake Fatuma Ally mkazi wa mtaa wa matankini mjini Masasi alisema hakuna ubishi kuwa kwa sasa Tanzania imepata kiongozi anayefanana na mwalimu Nyerere,mwenye msimamo na atakayeleta mabadiliko yenye tija kwa watanzania.

Alisema ahadi ya Rais Magufuli ya elimu bure pamoja na kufuta michango yote mashuleni imekuja wakati muafaka kwa kuwa wazazi wamekuwa na mzigo mkubwa wa michango hiyo na kudai kuwa hata hiyo fedha hawajui inafanya kazi gani kwenye shule hizo.

“Binafsi sio mshabiki wa chama chochote ila ukweli ni kwamba nimemfuatilia sana Rais Magufuli alipokuwa anaomba kura wakati wa kampeni…na nikabaini kuwa ni mtu mwenye dhamira ya kutuondolea umaskini na changamoto mbalimbali”alisema Ally.

Naye Ahmad Namtyoka mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kagera Halmashauri ya mji wa Masasi kupitia Chadema amempongeza Dk.Magufuli kwa hotuba yake na kuongeza kuwa imani yake kwake imeongezeka tofauti na hapo awali kwa kuwa mambo aliyoyaahidi wakati wa kampeni ameendelea kuyasisitiza kuwa atatekeleza.

Alisema wao kama viongozi wa kuchaguliwa na wananchi wanaomba nao walipwe mshahara au posho kama ilivyo kwa viongozi wengine kwani wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu huku wakikosa kuwa na vitendea kazi.

Aidha Mbaraka Rajabu alisema alitegemea hotuba ya Rais Magufuli itakuwa na maneno mengi ya kuisifu na kuipongeza serikali ya awamu ya nne lakini imekuwa ni tofauti kwani Dk.Magufuli alitumia muda mwingi wa hotuba yake kueleza atawafanyia nini watanzania kwa kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake.

Alisema ameipokea kwa mikono miwili hotuba ya Rais Magufuli hasa pale alipowataka wabunge kuacha tofauti zao za itikadi za vyama vyao na badala yake wafanye kazi huku akitoa uhuru kwa wabunge kuikosoa serikali yake pale itakapokosea.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top