Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU UCHOMAJI MOTO MISITU KWA WANANCHI WA MIKOA YA LINDI NA MTWARA.

TANGAZO
 MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwahutubia wakulima na wananchi kwa ujumla wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya wakulima Kitaifa yaliyofanyika Ngongo Manispaa ya mji wa Lindi.

Na Clarence Chilumba,Lindi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hasani amepiga marufuku uchomaji moto wa misitu katika mikoa ya Lindi na Mtwara lengo likiwa ni utunzaji wa mazingira.

Pia amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri katika mikoa hiyo kuhakikisha wanawasimamia wananchi wao katika kuachana na vitendo vya uchomaji wa misitu.
Marufuku hiyo ameitoa leo kwenye kilele cha siku ya wakulima (NANE NANE) kwenye viwanja vya Ngongo Manispaa ya Mji wa Lindi.


 Mbunge wa jimbo la Mtwara Vijijini Mheshimiwa Hawa Ghasia (Kulia) akicheza ngoma na kikundi cha Ngoma wakati wa maadhimisho ya siku ya wakulima.
 MAKAMU wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwenyekiti es Halmashauri ya Mji wa Masasi Mheshimiwa Sospeter Nachunga kwenye maonesho ya Nane Nane kitaifa 2016.
 WAZIRI wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Charles Tizeba akizungumza na wananchi wa Mikoa ya Lindi na Mtwara Kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wakulima kitaifa yaliyofanyika viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi.
 WANANNCHI wakisikiliza kwa makini Hotuba Mbalimbali za Viongozi katika maadhimisho ya siku ya wakulima.
WAZIRI wa Fedha Dk.Philip Mpango akiongea na wakazi wa mikoa ya Lindi na Mtwara.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top