Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

WIKI YA MAJI: ASILIMIA 81 YA WAKAZI WA MJI WA MASASI WANAPATA MAJI SAFI NA SALAMA

TANGAZO
Na Clarence Chilumba, Masasi TC.
Halmashauri ya mji wa Masasi inawahudumia wananchi wake kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama kupitia mtandao wake wa maji ambao kwa kiasi kikubwa umefika kila eneo la Halmashauri hiyo.

Mji wa Masasi ni mji ambao unawahudumiwa na vyanzo vya maji vya aina tatu ambavyo ni Mtiririko, Visima Virefu na Visima Vifupi.

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 Halmashauri ya mji wa Masasi ina wakazi 102,696 ambapo kati yao wanaopata huduma ya maji safi na salama ni watu  83,128 ambayo ni sawa na asilimia 81 ya wakazi wote wa mji huo.

Katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za maji, Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara katika mpango wake wa Bajeti ya maendeleo kwa mwaka wa fedha wa 2015/2016 imepanga kutumia jumla ya shilingi 647,600,000/= katika idara ya Maji.

Lengo la Halmashauri hiyo ni kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora ya maji safi na salama kwa wananchi wa vijiji vipatavyo 30 kwa asilimia 85.

Kupitia kiasi hicho cha fedha kilichopangwa kitumike Halmashauri ya Mji wa Masasi imakusudia kufanya mambo yafuatayo ili kuendana na mpango wa matokeo makubwa sasa maarufu (BRN) ikiwemo uchimbaji wa visima na uwekaji wa pampu katika vijiji vitano vya Chipole,Mpekeso,Magumuchila,Machenje na Mlundelunde.

Aidha Halmashauri hiyo kupitia mpango wa Bajeti hiyo imepanga kufanya ukarabati wa visima vitano vya maji katika vijiji vya Mkapunda, Mumbaka, Tukaewote, Mkarakate pamoja na Sululu ambapo pia imepanga kubadilisha mfumo wa genereta kuwa mfumo wa umeme jua katika kisima kilichoko Namkungwi.

Mipango mingine iliyopo ni ile ya kuwezesha ufungaji wa umeme jua kwa ajili ya usambazaji wa maji safi na salama kwa vijiji jirani kwa mabwawa ya Machombe na Namikunda pamoja na usimamizi na ufuatiliaji wa miradi hadi ifikapo juni 2016.

Aidha Mji wa Masasi unapata huduma zake za Maji kutoka kwa Mamlaka ya Maji Safi na Salama Masasi-Nachingwea (MANAWASA) mradi wenye lengo la kuwapatia wakazi wa mji wa Masasi huduma bora ya Maji safi na Salama.

Hii ni wiki ya maji yenye kauli mbiu isemayo “MAJI NA MAENDELEO ENDELEVU”.



TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top