Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

FAWOPA-TANZANIA YATOA MSAADA WA VIFAA VYA SHULE KWA WANAFUNZI WA SEKONDARI

TANGAZO
 Na Fatuma Maumba,Mtwara.
Wanasiasa mkoani Mtwara wametakiwa kuhamasisha wananchi  kuona umuhimu wa kuwapeleka watoto wao shule ili waweze kupata elimu ambayo itawasaidia katika maisha yao ya baadae kwa kupata ajira  kwa kuizngatia kuwa kwa sasa mkoa wa  Mtwara kuna uwekezaji mkubwa wa viwanda mbalimbali.

Aidha  wanasiasa wameaswa kutambua kuwa wana  jukumu kubwa la kuwahamasisha wananchi kupeleka watoto wao shule waweze kunufaika na matunda ya gesi kwa kupata ajira kwenye viwanda vitakavyojengwa mkoani humo.

Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Katibu Mtendaji wa Shirika la Faidika wote Pamoja la mkoani Mtwara( Fawopa-Tanzania), Baltazar  Komba, wakati natoa misaada mbalimbali ya vifaa vya shule kwa  wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu kutoka shule mbalimbali za sekondari mkoani Mtwara.

Alisema wanasiasa wanapaswa kushiriki ipasavyo katika  mapambano ya  kuhamasisha wananchi kupeleka watoto wao shule kama  kwa kuwa wananchi walio wengi hutegemea sana sauti ya wanasiasa  pindi wanapohitaji kufanya  maamuzi.

Kwa mujibu wa Komba alisema  Wabunge pamoja na madiwani wanapaswa kuliongelea suala la   elimu na kwamba ikiwezekana watunge sheria ndogo kuhusiana na masuala mazima yanayosababisha watoto  wengi kutoripoti shuleni.

“Tatizo kwa sasa hatusikii sauti zozote za kukemea tatizo hili kutoka kwa wabunge au madiwani   kama wanavyofanya Wakuu wa mikoa na Wakuu wa wilaya kuhamasisha wananchi kuwapeleka watoto wao shuleni”.alisema Komba.

Hata hivyo Komba, aliwalalamikia wazazi ambao watoto wao wanaishi katika mazingira magumu ambao wanasomeshwa na Shirika la Fawopa-Tanzania wanashindwa kufika ofisi za shirika hilo na kuwaunga mkono kwa juhudi zao za wanazofanya za kuwasomesha watoto wao.

 Alisema wazazi waunge mkono jitihada za Fawopa  kwa kuhakikisha watoto wao wanaenda shuleni  kwa kufuatilia mwenendo wao ikiwa ni pamoja na kukagua mahudhurio yao shuleni na ushiriki wa mtoto  katika tendo zima la  kujifunza.

Msaada waliopatiwa watoto hao ni pamoja na sare za shule,viatu, peni, penseli, madaftari makubwa pamoja na  mabegi ya shule kwa ajili ya kubebea madaftari yao.
Mwisho.

Katibu Mtendaji wa Shirika la Faidika wote Pamoja la mkoani Mtwara (Fawopa-Tanzania), Baltazar  Komba, akiwapatia msaada wa vifaa vya shule baadhi ya wanafunzi ambao wanaishi katika mazingira magumu kutoka shule mbalimba za sekondari mkoani Mtwara.







TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright 2025 Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top