Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

WANANCHI HALMASHAURI YA MJI MASASI WAOMBWA KUJITOLEA UJENZI WA MAABARA

TANGAZO
Na Clarence Chilumba,Masasi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji WA Masasi Mkoani Mtwara, Fortunatus Kagoro amewataka wananchi mjini humo kuwa na moyo wa uzalendo na mji wao katika kuchangia ujenzi wa maabara za shule za sekondari zilizopo kwenye Halmashauri hiyo.

Pia amemuomba mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Masasi Andrew Mtumusha kuwashawishi madiwani wa halmashauri hiyo kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa maabara.

Alitoa kauli hiyo jana wakati wa hafla fupi ya wadau wa maendeleo ya elimu iliyokuwa na lengo la kuchangia ujenzi wa maabara ili kuendana na agizo la Rais iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano katika shule ya sekondari ya  wasichana Masasi.

Alisema ni vyema kila mwana jamii wa mji wa Masasi akaona umuhimu wa kuchangia ujenzi wa maabara hizo ambazo ni watoto wa Masasi ndio watakaosoma ili baadae waje wafanye kazi katika viwanda vya gesi iliyogundulika mkoani Mtwara.

Kwa mujibu wa Kagoro alisema Halmashauri inayo jukumu la kufanya kwa nafasi yake lakini pia jamii kwa ujumla nayo ina nafasi yake katika kushiriki kwenye ujenzi wa maabara hizo zenye lengo la kupata wataalamu wa masomo ya sayansi.

“Maabara hizi tunazozijenga ni kwa ajili ya watoto wa Masasi…ambao hapo baadae watakuja kuwa madaktari na walimu wazuri wa masomo ya sayansi,hivyo jamii ni wajibu wenu kuchangia ujenzi wa maabara hizo”.alisema Kagoro.

Alisema kupitia madiwani ambao ndio wawakilishi wa kata ambamo maabara hizo zinajengwa wananchi waelimishwe na waombwe wawe na moyo wa kujitolea kwa kutumia nguvu kazi zao na wakatio mwingine hata michango ya fedha ama vifaa vya ujenzi.

Mkurugenzi huyo aliongeza kwa kusema kuwa kwa sasa nchini kumekuwa na ushindani mkubwa wa elimu mazingira yanayopelekea nafasi za ajira kuwa chache na zenye ushindani hivyo watoto wa Masasi wakisoma Masomo ya sayansi watakuwa ni miongoni mwa washindani wakubwa katika soko la ajira.

“Wakati Fulani nilitembelea mkoa wa Njombe nilifika kwenye nyumba ya kulala wageni…lakini katika hali ya kushangaza nilikuta tangazo la nafasi za kazi mlangoni wakihitaji mchinja kuku kwa masharti ya kuwa ni lazima awe amefikia kidato cha nne”.alisema.

Alisema suala la ujenzi wa maabara ni muhimu ambalo linahitaji msukumo mkubwa na kwamba kwa vyovote itakavyokuwa Halmashauri yake itajitahidi kukamilisha ujenzi wa maabara hizo.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na wageni mbalimbali jumla ya fedha shilingi milioni 90 zilihaidiwa kutoka kwa wadau wa maendeleo wa mji wa Masasi huku mahitaji yakiwa ni shilingi milioni 140.

Mwisho.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top