Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

HAWA GHASIA AWATAKA WAZAZI NA WALEZI MKOANI MTWARA KUWAPELEKA WATOTO WAO SHULENI

TANGAZO
Na Fatuma Maumba,Mtwara.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa Ghasia, amewata wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao shule ambao walibahatika kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Waziri huyo, alisema wazazi wanatakiwa kuwapeleka watoto wao shule kwani elimu ndio itakayosaidia waweze kunufaika na uchumi wa gesi ambao unakuja katika mkoa wa Mtwara.

 “Niwaombe tu wazazi wenzangu wawapeleke watoto wetu katika shule na wahakikishe waliochaguliwa wote wanaenda kidato cha kwanza na tusomeshe watoto kwa sababu elimu ndio itakayotusaidia tuweze kunufaika na uchumi wa gesi ambao unakuja katika mkoa wetu wa Mtwara bila kusomesha watu tutabaki kulalamika hata kama viwanda vitajengwa kwa mamia,” alisema Waziri Ghasia.

Alisema Kama watoto wa mikoa ya kusini hawatapata elimu basi wataishia kufanya kazi za chini sana ambazo hazina hadhi hivyo watashindwa kunufaika ambapo amewaomba wazazi kutilia mkazo suala la elimu kwa watoto wao.

“Ndugu zangu bila kujibana na kujinyima watoto wetu hawatasoma kwani wote sisi hapa tunaozungumza tulikuwa ni watoto wa wazazi wa kawaida sana lakini walijibana wakatusomesha na sasa hivi wanayaona matunda”. Alisema Ghasia.

Hata hivyo Waziri Ghasia ambaye pia ni Mbunge wa Mtwara Vijijini ameipongeza wilaya yake ya Mtwara Vijijini kwa kufanya vizuri katika matokeo ya kidato cha nne mwaka jana ila amewata wasibweteke na matokeo mazuri waliyoyapata na badala yake wakaze buti ili waweze kushika nafasi ya kumi ama ya tatu kitaifa.

 “Naomba niipongeze wilaya yangu ambayo imeshika nafasi ya pili na pia niupongeze Mkoa kwa ujumla kwa sababu mwaka 2013 mkoa wa Mtwara katika matokeo ya kidato cha nne tulikuwa wa tatu kutoka mwisho lakini mwaka 2014 tumekuwa wa kumi kitaifa…kwa hiyo kwa kweli tumesonga mbele sana lakini hata hivyo pamoja na pongezi hizi tusibweteke bado tuna kazi kubwa sana ya kufanya ili tuweze kufanya vizuri tena.

Waziri Ghasia, alisema siri ya mafanikio ya kufanya vizuri mwaka 2014 Kama alivyosema kwamba mkoa wa Mtwara kwa sababu walikuwa wa tatu kutoka mwisho Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliomba apate maelezo, kwa nini wameshika hiyo nafasi ya tatu kutoka mwisho na ajue mikakati yao ikoje ili kuhakikisha wanasonga mbele.

Kwa hiyo kama mkoa ilibidi utoe maelezo lakini huwezi kupeleka mikakati alafu usiitekeleze kwa hiyo walijiwekea mikakati na waliitekeleza na mwisho wa siku wakafanikiwa kushika kumi bora Kitaifa mwaka jana, lakini kitu kingine pia ni ushirikiano na kuthamini walimu katika maeneo yao.

Mwisho.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top