TANGAZO
Na Clarence
Chilumba, Masasi.
Jumla ya
wanafunzi 50 kutoka kwenye shule 10 za sekondari zilizopo katika Halmashauri ya
Mji wa Masasi mkoani Mtwara wameshiriki kwenye mdahalo mkubwa wa kielimu
uliokuwa na lengo la kujadili masuala yahusuyo taaluma uliofanyika kwenye
ukumbi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Masasi.
Akizungumza
jana wakati wa ufunguzi wa mdahalo huo Ofisa elimu taaluma kwa shule za
sekondari wa Halmashauri ya mji wa Masasi Upendo Rweyemamu alisema midahalo
hiyo ni miongoni mwa mipango mkakati ya
idara ya sekondari katika kukuza stadi ya uzungumzaji wa lugha ya kiingereza
ambayo imekuwa changamoto kwa wanafunzi wengi nchini.
Alisema baadhi
ya wanafunzi wa sekondari wamekuwa wakifanya vibaya mitihani yao ya kumaliza
kidato cha nne kutokana na kutoifahamu kwa ufasaha lugha ya kiingereza ambayo
ni lugha inayotumika katika ufundishaji wa masomo yote katika shule za
sekondari ukiondoa Kiswahili pekee.
Kwa mujibu wa
Rweyemamu alisema kuwepo kwa mpango huo wenye manufaa kwa wanafunzi pamoja na
Halmashauri kwa ujumla kunatokana na mshikamano uliopo kati ya idara ya elimu
ya sekondari,walimu wakuu wa shule hizo pamoja na walimu wao ambao wamekuwa na
msukumo mkubwa kwa wanafunzi kuweza kushiriki midahalo mbalimbali
inayoandaliwa.
“Wanafunzi
mnachotakiwa kujua ni kuwa hamko hapa kupoteza muda kwa kuwepo na kushiriki
kwenye mjadala huu wa leo…kuwepo kwenu hapa kutasaidi nyinyi wenyewe kuongeza
uelewa katika kuzungumza lugha ya kiingereza na nawaomba mjiamini,msiwe na hofu
pale mtakapopata nafasi ya kuchangia mjadala huu”,alisema Rweyemamu.
Aidha Rweyemamu
alitumia nafasi hiyo kuwashukuru na kuwapongeza wakuu wa shule pamoja na walimu
wote wa shule hizo hasa wale wanaofundisha masomo ya kiingereza kwa jitihada
kubwa wanazozifanya kwenye shule zao ambazo matunda yake yameanza kuonekana kwa
baadhi ya wanafunzi kufanya vizuri kwenye mitihani yao ya kidato cha nne.
Katika mdahalo
huo mada kuu iliyojadiliwa ni “wanafunzi wa kike wa sekondari wanapaswa kuendelea
na masomo hata baada ya kupata ujauzito” mada iliyoibua hisia na mvutano mkali
kwa kundi lililokuwa linaunga mkono hoja na lile lililokuwa linapinga hoja huku
makundi yote yakionekana kutoa michango yenye tija kwa mwanafunzi wa kike.
Kwa upande wake
mratibu wa mdahalo huo mwalimu Humud Mpende mkuu wa shule ya sekondari ya
Mtandi alisema jitihada zinazofanywa na walimu wa shule za sekondari
Halmashauri ya mji wa Masasi zinapaswa kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa
elimu na halmashauri kwa ujumla.
WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI YA MTANDI
Alisema
midahalo hiyo ni mwendelezo ambao tangia mwaka jana wamekuwa wakifanya midahalo
hiyo mara kwa mara ili kukuza stadi za kuzungumza lugha ya kiingereza sambamba
na kumpa mwanafunzi uwezo wa kujiamini na namna ya kuwasilisha mada mbele ya
hadhira.
Mwisho.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD