Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

VIONGOZI WA KIMILA (Mamwenye) WAMLILIA ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA MASASI FARIDA MGOMI.

TANGAZO
Na Clarence Chilumba, Masasi.
Viongozi wa kimila maarufu Mamwenye wa wilaya ya Masasi mkoani Mtwara wameelezea kusikitishwa kwao na uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete wa  kumwamisha  aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Masasi Farida Mgomi na kumpeleka wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.

Pia walishindwa kuficha hisia zao baada ya kueleza kuwa mkuu huyo wa wilaya anayeondoka ndie aliyefanikisha kwa wao kutambuliwa na viongozi wa serikali na chama kwa ujumla tofauti na hapo awali ambapo walidharauliwa na hawakupewa thamani yoyote kwa kigezo kuwa wazee hawana jipya.

Akizumgumza jana kwa niaba ya wazee hao wa kimila, wakati wa hafla fupi ya makabidhiano na mkuu mpya wa wilaya ya Masasi katibu wa viongozi hao wa kimila wilaya ya Masasi Mwenye Nakaruma Mchopa alisema kamwe hawatamsahau mkuu huyo wa wilaya anayeondoka kwa kuwa alikuwa karibu sana na viongozi hao na aliwapa nafasi ya kutoa ushauri kwa serikali ya wilaya ya Masasi.

Alisema wakati anateuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Masasi alikuta wilaya hiyo ikiwa na changamoto nyingi kama vile tatizo la njaa,maji,mimba za utotoni pamoja na ukiukwaji wa maadili kwa vijana changamoto ambazo amekiri kuwa kwa sasa zimebaki kuwa historia kwa wilaya hiyo kutokana na umoja na mshikamano kati ya serikali na viongozi wa kimila.

“Sisi Mamwenye tuko hapa Masasi toka zamani…lakini hatujawahi kushirikiana na serikali ya wilaya kama tulivyoshirikiana na mkuu huyu wa wilaya anayeondoka,tulinyanyaswa na kudharauliwa mbaya zaidi hatukuwa na umoja wetu lakini mara baada ya yeye kuja Masasi aliweza kutuunganisha na tukaunda umoja wa Mamwenye”.alisema Mchopa.

Kwa mujibu wa katibu huyo wa viongozi wa kimila wilaya ya Masasi alisema wakati wa uongozi wa Farida viongozi hao aliwapa fursa ya kukutana ana kwa ana na viongozi wa juu wa serikali akiwemo Rais Jakaya Kikwete alipofanya ziara ya kikazi wilayani Masasi kitu ambacho hapo awali hakikuwepo.

Alisema viongozi wa kimila wana nafasi kubwa katika jamii yoyote nchini katika kutoa elimu ya maadili lakini katika wilaya ya Masasi hawakuwahi kupewa kipaombele na badala yake walionekana kuwa ni miongoni mwa watu wasioenda na wakati kulikosababisha jamii kuishi kinyume na maadili ya kitanzania.

“Hatuna cha kukulipa kwa haya yote uliyotufanyia zaidi ya kukuombea maisha marefu na mafanikio makubwa katika uongozi wako… tunaamini ipo siku utakuja kuwa mkuu wa mkoa wa Kusini ambao mchakato wake wewe ndiye uliyeuanzisha”.alisema.

Kwa upande wake mkuu huyo wa wilaya anayehamia wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma aliwashukuru viongozi hao wa kimila kwa ushirikiano waliompatia kwa kipindi chake chote cha miaka mitatu ya uongozi akiwa mkuu wa wilaya ya Masasi mazingira yaliyopelekea kuendelea kuaminiwa na Rais.
Mwisho

 Aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Masasi Farida Mgomi akipeana mkono na mkuu mpya wa wilaya ya Masasi Bernald Nduta wakati wa hafla fupi ya  makabidhiano ya ofisi.
 "Mimi naondoka naelekea wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma Lakini naiacha wilaya ya Masasi ikiwa salama lakini hii yote ni kutokana na ushirikiano wangu na kamati ya ulinzi na usalama...nakuomba endeleza mahusiano hayo".Farida Mgomi.
Mkuu mpya wa wilaya ya Masasi Bernald Nduta akitoa neno la shukrani kwa mkuu wa wilaya anyeondoka Farida Mgomi.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top