Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

SHEIKH MKUU WA MKOA WA MTWARA AWAASA WATANZANIA KUTOICHEZEA AMANI

TANGAZO
Sheikh Nurdin Abdallah Mangochi
Na Fatuma Maumba,Mtwara.
WATANZANIA  wametakiwa kuendeleza na kudumisha amani, upendo, mshikamano na umoja waliokuwepo nao miaka yote, hasa kipindi hiki Taifa linapoelekea kwenye mchakato mzima wa kura za maoni pamoja na Uchaguzi Mkuu unawajumuisha Madiwani,Wabunge, na Rais.

Ushauri huo umetolewa hivi karibuni, mjini hapa na Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mtwara,Sheikh Nurdini Mangochi, wakati akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi  wa BAKWATA mkoa. 

Alisema suala la amani,upendo , mshikamano umoja si la Serikali tu, hata mtu mwenyewe akiwa nyumbani kwake anatakiwa awe na amani na upendo na familia yake.

 “Suala la amani, upendo, mshikamano na umoja si suala la Serikali pekee hata wewe mwenyewe unapokuwa nyumbani kwako unatakiwa uwe na amani na upendo na familia yako…kwa hiyo mimi naomba watu wote Tanzania Nzima  ambao watagombea nafasi ya Udiwani, Urais na Ubunge basi watangulize mbele amani ndio msingi wa maisha kwani kama hakuna amani shughuli zote zinasimama na watu hawatafanya kazi kwa uhuru, kama kiongozi wa dini basi nasisitiza amani itawale siku zote katika maisha yetu. 

Pamoja na mambo mengine  Sheikh Mangochi, alisema  kwamba kiongozi yoyote hapa duniani kitu cha kwanza anachotakiwa afanye ni kusimamia na kuzingatia maadili ya kazi yake ndipo ataendesha vizuri uongozi wake.

Alisema kuwa sehemu yeyote ile ya kazi ukisikia kuna migogoro basi kiongozi amekiuka maadili ya kazi yake, kwa hiyo ni vizuri viongozi wakafuata maadili ya kazi zao ili kuepusha migogoro isiyokuwa ya lazima sehemu za kazi.

“Tendo la maadili hilo ndio kubwa sehemu ya kazi, ukisikia kelele nyingi kwenye maofisi basi  ujue kuna kiongozi amekosa maadili,  hata nyinyi waandishi wa habari mkikosea maadili ya kazi yenu tu basi mtasikia watu wanawalalamikia…kwa hili hata mimi namuomba Mwenyezi Mungu anipe uwezo mzuri  nisimamie maadili katika huu uongozi wangu.

Kwa upande wake aliyekuwa Mwanyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu mkoa wa Mtwara, Alhaji Marijani Dadi, alisema kwamba katika miaka yake kumi ya uongozi  wa Baraza hilo, Waislamu wote wa mkoa wa Mtwara walikuwa kitu kimoja, na amewataka waendeleze mshikamano huo uliokuwepo tokea mwanzo.

“Nimekaa madarakani kwa miaka kumi na katika kipindi chote hicho Waislamu wa Mtwara tulikuwa kitu kimoja na wilaya zake zote sita hakuna tatizo lolote, leo nakabidhi na husia wangu mkubwa kwa ninaowakabidhi waendeleze mshikamano wilaya zote ziwe kitu kimoja isiwe watu wa sehemu fulani wanawatenga wengine,” alisema Alhaji Dadi na kuongeza:
“Vile vile tuzingatie maendeleo ya nchi yetu kwa sababu kuna michakato mbalimbali sisi kama raia wa nchi hii tuna haki ya kushiriki, kwa mfano sasa hivi kuna mambo ya Katiba lazima na wao wasimamie waone kwamba Katiba inafanikiwa kwa maana watu wajitokeze kwenda kupiga kura zao ili kutoa maoni yao… Kikubwa ninachohimiza  ni kwamba utulivu hauji bure bure  kwani wanaodumisha utulivu ni wananchi wenyewe na sisi ni sehemu katika raia wa nchi hii ni lazima tuhakikishe tunatimiza wajibu wetu ili utulivu na amani si kwa Mtwara tu basi uambukize na sehemu nyingine.
 Mwisho.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright 2025 Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top