Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MTWARA AWAFUNDA WAANDISHI WAKE.

TANGAZO
Mwenyekiti wa MTPC Hassan Simba
Na Fatuma Maumba,Mtwara
 Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuandika habari za vijijini ambazo zimekuwa haziandikwi kwa kiwango kinachostahili na badala yake wamekuwa wakiandika habari nyingi za mjini  kuliko za vijijini.

Hayo yalisemwa hivi karibuni, mjini hapa na Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa Habari mkoani Mtwara (MTPC), Hassani Simba, wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa katika kikao cha kawaida cha kukumbushana juu ya utendaji kazi wa waandishi hao.

Aidha,Simba alieleza kwamba waandishi wengi wamekuwa wakijikita kuandika habari za mjini pekee wakati kuna kundi kubwa la watu ambalo linaishi vijijini likikosa huduma mbalimbali za kijamii, hususani afya , miundombinu na maji safi na salama.

Alisema wanahabari wanauwezo mkubwa sana wa kuandika habari za vijijini na wakaibua matatizo makubwa sana na changamoto zake katika jamii lakini watu hao wamewasahau kabisa kuandika habari zao .
“Waandishi wa habari tumewasahau wananchi wanaoishi vijijini tukumbuke ya kwamba kundi hili wanatutegemea sisi tupamze sauti zao kwa kuwaandikia matatizo walikuwa nayo, kwani wao hawana sehemu pa kusemea zaidi ya kututegemea sisi kuibua matatizo yao” Alisema Simba.

Simba alisisitiza ya kwamba waandishi wa habari pia wakumbuke kuandika habari zenye uwiano sawa habari za mjini na vijijini bila kuleta upendeleo  wowote hule kwani watakapoandika usawa habari hizo zitaleta furaha kwa kundi hilo ambalo limesahaulika na kujiona kwamba nao wanathaminiwa.

Ikumbukwe ya kwamba kundi kubwa linaloishi vijijini wengi wao ni maskini na hawana sauti kabisa kwaiyo ni jukumu lao wao kama waandishi wa habari kuwasemea wananchi wasiokua na sauti  kwani jamii hiyo inawategemea sana wanahabari kwa asilimia mia moja.

Simba alisema, hakuna sehemu yoyote ile ambayo inayoendelea ama kupata mafanikio bila kuwa na vyombo vya habari kwa hiyo naomba wajitaidi sana wanahabari kuandika habari za vijijini ili kuleta maendeleo sehemu hiyo.
“Tunapaswa kuwafikia wananchi ambao wanaishi vijijini wanaohitaji habari za kusoma  kwenye magazeti, kusikiliza redio na kutazama Luninga juu ya taarifa zao za vijijini ili kuweza kupata motisha ya maendeleo yao kiujumla” Alisema Simba.
 Mwisho.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright 2025 Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top