Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MURJI AWATAKA WAZAZI MKOANI MTWARA KUWALEA WATOTO WAO KATIKA IMANI YA DINI

TANGAZO
Fatuma Maumba, Mtwara.
 Wananchi mkoani Mtwara wametakiwa kuwalea watoto wao kwenye malezi ya dini ya kiislamu ili waweze kujengeka kimaadili, hatua itakayowawezesha kukubalika katika jamii ya watu waliostaarabika.

Ushauri huo umetolewa na Mbunge wa jimbo la Mtwara Mjini, Hasnain Murji, wakati wa mazungumzo yake na waumini wa dini ya kiislamu eneo la Mmart Chuo cha kilimo Mtwara, ambapo pamoja na mambo mengine amechangia shilingi laki tano na mifuko hamsini ya saruji kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa madrasa ya watoto ambao kwa hivi sasa wanatumia darasa ambalo halifai kusomea.

Alisema ni vizuri jamii ikatambua na kuelewa umuhimu wa kuwalea watoto wao kwenye maadili mema ya dini ya kiislamu ambayo yataweza kuwasaidia katika maisha yao ya baadae, kutokana siku hizi wototo wengi wamekuwa wakikiuka maadili ya dini zao.

“Mimi nina imani kabisa kijana yeyote yule ambaye amesoma kwenye madrasa ama amelelewa kwenye dini ni tofauti sana na vijana wa kwetu ambao wako mitaani…Ndugu zangu tunapata shida sana na vijana ambao hawajaelimishwa kidini.

“Lakini nawahakikishia Mtwara hii vijana ambao waliokuwa na elimu na wasiokuwa na elimu wanaweza kuja kupata hifadhi lakini mtu asiyekuwa na elimu hana nidhamu au wewe una elimu huna nidhamu bado nafasi utakosa, kwa sababu wenzetu wanaotoka nje wataangalia maadili kwanza kwa hiyo lazima tuwalee watoto wetu kwa kuzingatia maadili ya dini ya kiislam,” alisema Murji.

Kwa upande wake Mwalimu wa Madrasa, Hamadi Mbwana, alimshukuru Mbunge wa Mtwara, Hasnain Murji kwa msaada alioutoa kwani utapunguza changamoto waliokuwa nazo wa ujenzi wa madrasa ya watoto.

Mwisho.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright 2025 Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top