Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MAMA SALMA KIKWETE AKABIDHI MSAADA WA GARI LA WAGONJWA HOSPITALI YA MKOMAINDO

TANGAZO
Gari la wagonjwa lililotolewa na Mama Salma Kikwete.

Na Clarence Chilumba,Masasi.
Mke wa Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake na maendeleo nchini (WAMA) Salma Kikwete leo ametoa msaada wa gari moja ya wagonjwa katika hospitali ya Mkomaindo Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara.

Msaada huo wa gari la wagonjwa alioutoa ni kutoka kwenye mfuko wa taasisi ya WAMA kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la Sayeed Corporation ikiwa ni utaratibu wake wa kawaida katika kushughulikia mahitaji ya msingi ya akinamama na watoto hapa nchini.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo alisema kupatikana kwa gari hilo ni kielelezo tosha cha upendo mkubwa walionao shirika la Sayeed Corporation kwa wananchi wa mji wa Masasi kwa kuwa takwimu zinaonesha kuwa akinamama wajawazito hupoteza maisha kutokana na kucheleweshwa kufika katika vituo vya huduma za uzazi.

“Niliamua kukabidhi gari hili kwenye Hospitali ya Halmashauri ya mji wa Masasi, baada ya kubaini kuwa akinamama wengi wanahitaji huduma ya usafiri ili kuja katika hospitali hiyo kwa wakati”.Alisema Salma.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo wa WAMA alisema Hospitali ya Mkomaindo ni miongoni mwa hospitali kongwe nchini ambayo imekuwa ikishirikiana na hospitali zingine zikiwemo hospitali za wilaya za Nachingwea,Lindi,Newala,Mtwara pamoja na nchi jirani ya Msumbiji na kwamba kupatikana kwa gari hiyo kutasaidia kuleta wagonjwa wanaotoka katika maeneo hayo.

Gari la Wagonjwa lililotolewa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete kwa Hospitali ya Mkomaindo Halmashauri ya mji wa Masasi.

Alisema Taasisi ya wanawake na Maendeleo (WAMA) ilianzishwa ikiwa na malengo ya kuboresha afya ya uzazi ya mama na mtoto kwa kununua na kutoa misaada ya vifaa vya afya katika hospitali mbalimbali nchini, kufanya kampeni ya kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Aidha mikakati mingine iliyowekwa na taasisi hiyo ni pamoja na kuendesha kampeni za kufanya uchunguzi wa saratani ya matiti n ile ya mlango wa kizazi sambamba na kutoa elimu kwa waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla juu ya umuhimu wa afya ya uzazi salama.

Alisema akinababa pia wanapaswa kuwa karibu na wake zao kwa kuwafanyia maandalizi ya rasilimali fedha kwa kuwa vifo vingi vya wanawake na watoto hutokana na wananchi wengi kushindwa kuwapeleka hospitali kwa wakati akinamama wanaoshindwa kujifungua kwa njia ya kawaida.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia wananchi wa mji wa Masasi (Hawapo Pichani) kwenye viwanja vya Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Masasi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Masasi Andrew Mtumusha alimshukuru mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete kwa kuwapa msaada huo wa gari ya wagonjwa litakalotumika katika wilaya ya Masasi.

Alisema msaada huo umekuja kwa wakati na kwamba utakuwa umeokoa vifo vingi vya wanawake wajawazito na watoto vilivyokuwa vinatokea hapo awali kwa kucheleweshwa kufika kwenye vituo vya afya pamoja na hospitali ya Mkomaindo kwa wakati.
Mwisho.
 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Masasi Andrew Mtumusha akitoa shukrani zake kwa mwenyekiti wa Taasisi ya maendeleo ya wanawake (WAMA) mara baada ya kupokea msaada wa gari moja la wagonjwa.

 Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkomaindo Dkt.Albano Nditi akipeana mkono na mke wa Rais Mama Salma Kikwete baada ya kukabidhi taarifa ya Hospitali ya Mkomaindo.
 Mama Salma Kikwete akiangalia ndani ya gari hiyo aliyoitoa kwa hospitali ya mkomaindo Masasi.
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Masasi akiwa ameshika Funguo ya gari hilo la wagonjwa mara baada ya kukabidhiwa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
 Pichani ni vifaa vilivyopo ndani ya Gari hilo la Wagonjwa 
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa kwenye picha ya Pamoja na baadhi ya watumishi wa ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara.
 Mwenyekiti wa Taasisi ya Maendeleo ya Wanawake (WAMA) Mama Salma Kikwete akitia saini kwenye kitabu cha wageni katika hospitali ya mkomaindo Masasi mara baada ya kuwasili hospitalini hapo.
 Mama SALMA KIKWETE akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa kimila (MAMWENYE)
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwapungia mkono wananchi pamoja na wanafunzi waliojitokeza kumlaki alipowasili kwenye viwanja vya Ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Masasi.
 Mama Salma Kikwete akimuangalia mtoto katika wodi ya uzazi katika hospitali ya mkoamindo alipofanya ziara ya kuona wakinamama hao.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Masasi Andrew Mtumusha akipeana mkono na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete mara baada ya kumkabidhi gari ya wagonjwa.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright 2025 Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top