Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MTOTO WA MIAKA 14 ATUPWA JELA MIAKA 3 KWA KUMLAWITI MTOTO MWENZAKE WA MIAKA 9

TANGAZO
Na Clarence Chilumba,Masasi.
MTOTO mwenye umri wa miaka 14 (Jina linahifadhiwa) mkazi wa Njenga- Ndanda Halmashauri ya wilaya ya Masasi mkoani Mtwara amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kosa la kulawiti.

Mbele ya mwendesha mashtaka Iddi Athumani alidai mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo mwishoni mwa septemba, 2014 majira ya saa 11:30 jioni huko katika kijiji cha Njenga Ndanda Halmashauri ya wilaya ya Masasi mkoani Mtwara.

Athumani aliieleza Mahakama kuwa mshtakiwa huyo kwa makusudi alimlawiti mtoto mwenzake wa miaka tisa (Jina linahifadhiwa) anayesoma darasa la pili katika shule ya msingi Ndanda Halmashauri ya wilaya ya Masasi.

Alidai kuwa upelelezi umekamilika na unaonesha mshtakiwa alitenda kosa hilo ila kwa kuwa mshtakiwa ni mtoto aliiomba mahakama kumpunguzia adhabu ambapo aliomba kuwa mtoto huyo apelekwe kwenye gereza la wafungwa la watoto.

Baada ya  maelezo ya upande wa mashtaka hakimu wa mahakama ya wilaya ya Masasi Halfani Ulaya  aliridhika na maelezo yaliyotolewa na upande huo na kumtia  hatiani mshtakiwa huyo kwa kumpa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu jela .

Aidha mahakama ilitoa agizo kwa daktari wa wilaya kumfanyia vipimo vya afya mtoto huyo huku Ofisa maendeleo ya jamii pamoja na wazazi wa mtoto huyo wakitakiwa kutoa taarifa za maendeleo ya ukuaji wake kabla hajasafirishwa kuelekea mkoani Morogoro liliko gereza la watoto.
Mwisho.




TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top