Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

MILIONI 85 ZATUMIKA KULIPA KAYA MASKINI HALMASHAURI YA MJI WA MASASI.

TANGAZO

 Na Clarence Chilumba, Masasi.
Jumla ya shilingi milioni 89 zimetumika kwenye mpango wa kunusuru Kaya maskini sana kupitia awamu ya tatu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF III katika Halmashauri ya mji wa masasi mkoani Mtwara huku wanufaika na mpango huo wakielezea furaha yao.

Hayo yalisemwa jana  na mratibu wa Tasaf Halmashauri ya mji wa Masasi Joram Msyangi wakati wa zoezi la ugawaji wa fedha kwenye kaya masikini mjini humo ambapo amewataka wanufaika na mpango huo kutumia fedha wanazozipata kwa malengo yaliyokusudiwa na yenye tija kwa ustawi wa jamii.

 Alisema baadhi ya wanufaika wa mpango huo wamekuwa wakitumia fedha hizo kwa matumizi yasiyo na maana ikiwemo ulevi kitu ambacho kinakwenda kinyume na malengo ya mfuko wa maendeleo ya jamii ambayo lengo lake ni kuzinusuru kaya masikini
kama ilivyokusudiwa na kwamba kufanya kinyume na malendo ya mpango ziweze kuishi vizuri.

Alisema wanufaika wanapaswa kutambua kuwa ruzuku hiyo wanayopewa na serikali inapaswa kutumika huo ni kukosa shukrani kwa serikali ambayo ina nia ya kuboresha maisha ya wananchi wake.

Kwa mujibu wa mratibu huyo alisema Halmashauri ya mji wa Masasi imekuwa ikitekeleza miradi ya Tasaf kwa kiwango cha hali ya juu na kwamba wanatarajia kufikia malengo yaliyowekwa na serikali ya kuhakikisha kuwa kila mtanzania anakuwa na maisha bora kupitia ruzuku hizo pamoja na miradi mbalimbali ya maendeleo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wanufaika wa mpango huo Rukia Bakari(55),wa kitongoji cha Kagera,Hadija Rashidi(40) pamoja na Maria Mrope (66) wote wa kitongoji cha Wapiwapi B waliupongeza mpango huo ambao umekuwa ukiwasaidia kwa kiasi kikubwa katika kujikimu na maisha yao.
Mwisho.



Baadhi ya wanufaika waliokuwa wakisubiri kulipwa Ruzuku zao 
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright 2025 Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top