Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO
MIKOPO YAFAIDISHA WANAWAKE MASASI
Na Clarence Chilumba, Masasi.

Vikundi 11 vya wanawake wajasiliamali vilivyopo Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara vilivyopewa mkopo wa fedha shilingi milioni saba kutoka mfuko wa Taifa wa maendeleo ya wanawake wenye lengo la kuboresha maisha ya wanawake hapa nchini vimeanza kunufaika na mikopo hiyo.

Aidha baadhi ya vikundi hivyo hadi sasa vimeweza kuanzisha shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ikiwemo utengenezaji wa batiki, makapu, kofia, vitambaa, pamoja na mazulia ya majumbani mazingira yatakayosaidia wanawake hao kujiondoa kwenye wimbi la umaskini.
Pia baadhi ya vikundi hivyo vimekuwa vikijihusisha na shughuli za kilimo,biashara pamoja na ufugaji wa kuku na kanga ili waweze kupata fedha za marejesho ili vikundi vingine vya wanawake kama wao viweze kupatiwa fedha hizo ili nao waweze kunufaika kupitia mikopo hiyo yenye riba nafuu.
Hayo yalibainika wakati wa ziara maalumu jana ya ukaguzi wa vikundi hivyo uliofanywa na maofisa kutoka idara ya maendeleo na ustawi na jamii Halmashauri ya mji wa Masasi iliyokuwa na lengo la kujionea bidhaa zinazozalishwa na vikundi hivyo.
Akizungumza mara baada ya ziara hiyo Kaimu ofisa ustawi wa jamii Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani humo Pendo Malimilo alisema vikundi vingi kati ya hivyo 11 vilivyopewa mikopo vimeweza kufikia malengo na mikakati iliyojiwekea ikiwemo ya kupambana na umaskini.
Alisema baadhi ya vikundi bado vinaonekana kusuasua katika utekelezaji wa yale mambo ya msingi waliyokubaliana nao hivyo endapo vitaendelea na utaratibu huo basi havitaingizwa kwenye orodha ya awamu ya pili ya mikopo hiyo kwa kuwa vitakuwa vimeshindwa kutimiza viogezo na masharti ya mikopo hiyo.
Malimilo alisema katika ukaguzi huo wamebaini mapungufu kadhaa kwenye vikundi hivyo ambayo ni lazima wayatafutie ufumbuzi kwa lengo la kuwasaidia akinamama hao.
Moja ya vikundi vilivyotembelewa katika ziara hiyo ni pamoja na kikundi cha chama cha wajane Masasi (Chawamasi) ambacho hadi sasa kimeweza kupata faida iliyopo benki kiasi cha shilingi milioni 3 na kwamba shughuli kubwa wanazozifanya ni ufumaji wa vitambaa, kofia pamoja na mazulia.
Katibu wa kikundi hicho cha Chawamasi Monika Chigogoro alisema licha ya mafanikio hayo bado wanakabiliwa ni changamoto kubwa ya maneno ya kashfa na kejeli kutoka kwa akinamama wenzao kuwa wanachama wa kikundi hicho wengi wao ni wale wanaoishi na virusi vya Ukimwi kutokana na waume zao kufariki dunia.

Mwisho. 
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top