Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO
WANUSURIKA KIFO AJALINI









Na Clarence Chilumba, Masasi.
Abiria zaidi ya 20 wamenusurika kifo kufuatia gari waliyokuwa wakisafiria Toyota Hiace kutoka Mangaka wilayani Nanyumbu kuja Masasi mkoani Mtwara kuigonga kwa nyuma Bajaj na hatimaye kuacha njia kwenye eneo la makutano ya barabara ya Mtwara-Masasi.
Ajali hiyo imetokea jana majira ya saa 6:00 mchana ambapo gari lenye namba za usajili T 843 BVW Toyota Hiace lililokuwa likiendeshwa na dereva Juma Mzee (55) mkazi wa Masasi kuigonga kwa nyuma Bajaj yenye namba T 351 CMT ikiendeshwa na Alouter William (36) mkazi wa Masasi.
Mkuu wa polisi wilaya ya Masasi mkoani hapa Ndagile Makubi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa   ajali hiyo ilitokea jana majira saa 6:00 mchana katika eneo la makutano ya barabara itokayo Mtwara kuja Masasi ambapo gari hiyo iliigonga kwa nyuma Bajaj iliyokuwa inajaribu kuvuka kuelekea upande wa pili.
Alisema  gari hiyo lililokuwa na abiria zaidi ya 20  lilikuwa likitokea Mangaka wilayani Nanyumbu  kuja mjini Masasi  na kwamba lilipofika katika eneo la makutano ya barabara  karibu na ofisi za Tanesco  liliigonga kwa nyuma Bajaj na kuburutwa kuelekea eneo la Skaba.
 Makubi alisema abiria wote pamoja na dereva waliokuwa kwenye gari hiyo hakuna aliyejeruhiwa na kwamba dereva wa Bajaj alipata michubuko kidogo begani ambapo alitibiwa katika Hospitali ya Mkomaindo na hali yake inaendelea vizuri.
Katika hatua nyingine gari ndogo lenye namba za usajili T 445 CMF Toyota Cresta lililokuwa likiendeshwa na Christopher Gama (26) mkazi wa mtaa wa Maendeleo liliigonga ubavuni Bajaj yenye namba za usajili T 628 CGA likiendeshwa na Hamis Athumani (21) mkazi wa mtaa wa mkuti.
Katika ajali hiyo hakuna aliyejeruhiwa na kwamba chanzo cha ajali hizo zote ni uzembe na kukosa umakini kwa madereva wa vyombo hivyo vya moto.

Mwisho.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top