Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO

DC MASASI AWAPONGEZA REA
Na Clarence Chilumba, Masasi.
Mkuu wa wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Ajati Farida Mgomi amewapongeza wakala wa nishati vijijini kwa programu yao ya mafunzo inayoendelea wilayani humo itakayosaidia kukabiliana na uharibifu wa mazingira ya bahari.
Aidha mpango huo wa REA una lengo la kuhakikisha kuwa malengo ya MKUKUTA ya kufikisha nishati bora na yenye uhakika ya umeme kwa wananchi waishio vijijini inafanikiwa ifikapo mwaka 2015.
Hayo aliyasema juzi wakati anafungua mafunzo ya siku tano ya ukaushaji wa samaki kwa kutumia nishati ya jua yaliyoshirikisha washiriki 20 kutoka Somanga wilaya ya Kilwa mkoani Lindi katika ukumbi wa chuo cha maendeleo ya wananchi mjini Masasi.
Alisema mafunzo hayo yatachangia kuboresha shughuli za uvuvi kwenye maeneo ya bahari ya Hindi hivyo kukuza soko la samaki na kuchangia maendeleo kwa jamii kwa lengo la kupungzua umaskini wa kipato kwa wananchi.
Mgomi alisema matumizi ya nishati ya jua katika ukaushaji samaki kutaboresha ubora wa samaki hao na bidhaa zingine zitakazokaushwa kwa kutumia teknolojia hiyo ambapo ametoa wito kwa washiriki hao kutumia fursa hiyo ya mafunzo kikamilifu.
Alisema hatua ya wakala wa nishati vijijini ya kuandaa mafunzo hayo ya matumizi ya nishati ya jua italisaidia taifa kuondokana na uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji miti katika ukaushaji wa mazao kama vile ya samaki, matunda pamoja na mbogamboga.
Wakizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo  Yusuph Kitelebu ambaye ni msimamizi wa rasilimali za bahari (BMU) pamoja na Hamida Mjanaeli ambaye ni mhitimu wa shahada katika chuo cha ustawi wa jamii Dar es salaam walisema kuwa matarajio yao katika mafunzo hayo ni kupata elimu ya ukaushaji samaki kwa kutumia nishati ya jua.
Walisema kuwa changamoto kubwa iliyopo kwa wananchi wengi hapa nchini ni kuona kuwa rasilimali zilizopo ni zawadi kutoka kwa mungu mazingira yanayopelekea wengi wao kutolinda na kutunza rasilimali hizo.
Kwa upande wake mkuu wa chuo cha maendeleo ya wananchi Masasi ambaye pia ndiye mwezeshaji wa mafunzo hayo Fred Mwakagenda alisema ukaushaji wa samaki kwa kutumia nishati ya jua ni njia muafaka ya kuboresha mazao ya samaki hapa nchini.
Mwisho.






TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top