Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO

MASASI WAKAMILISHA MAABARA ASILIMIA 81
Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara imekamilisha ujenzi wa maabara katika shule zake za sekondari zilizopo kwenye halmashauri hiyo kwa asilimia 81 ili kutekeleza agizo la Raisi lililozitaka shule zote za sekondari za serikali hapa nchini kuwa na maabara tatu.
Pia Halmashauri hiyo kwa kutumia vyanzo vyake vya mapato vya ndani tayari imeshapeleka fedha shilingi milioni 15 kwa shule ambazo hazijamaliza ujenzi huo wa maabara lengo likiwa ni kukamilisha ujenzi huo mwishoni mwa Desemba 25 mwaka huu.
Akizungumza jana na waandishi wa habari wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa  maabara kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Masasi Henry Kagogoro alisema Halmashauri hiyo imejipanga kutekeleza agizo la Raisi kwa asilimia 100 mwishoni mwa desemba mwaka huu.
Alisema kati ya vyumba 27 vya maabara vinavyohitajika ni vyumba vitano pekee ndivyo ambavyo hadi sasa ujenzi wake unaendelea na kwamba vingi kati ya hivyo viko kwenye hatua nzuri ya umaliziaji huku vyumba vingine vikiwa katika hatua ya upandishaji wa kuta zake.

Alisema miongoni mwa shule tisa za sekondari zilizopo ndani ya Halmashauri hiyo saba tayari zimekamilisha huku mbili zikiendelea na ujezni huo na kwamba baadhi ya vyumba vya maabara hizo zimeshaanza kutumika huku zingine zikisubiri vifaa pamoja na samani.

Kagogoro alisisitiza kuwa ili kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo kwa wakati amepanga ratiba maalumu ya kila siku kwa wakuu wa idara na vitengo ambao wanatakiwa kufuatilia hali halisi ya ujenzi wa maabara hizo badala ya kusubiri taarifa wakiwa ofisini.

Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi huyo alisema kuwa hali ya ujenzi wa maabara katika Halmashauri hiyo ni nzuri huku akitoa wito kwa wakuu wa shule,bodi za shule pamoja na jamii kwa ujumla waunge mkono jitihada zinazofanywa na halmashauri katika kuhakikisha kuwa kila shule inakuwa na maabara za masomo ya sayansi.
“Kimsingi wanahabari, hatua tuliyofikia kwa sasa ni nzuri ingawa bado tunayo kazi kubwa ya kufanya katika hili…tumejipanga kikamilifu na kwamba tutahakikisha kuwa tunakamilisha ujenzi wa maabara zetu ili kutekeleza agizo la Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania”.Alisema.
 Alisema mikakati iliyopo ni kuimarisha miundombinu katika maabara hizo ikiwemo maji, kemikali pamoja na vifaa vingine muhimu vinavyotumika katika maabara kwa lengo la kuwajengea uwezo na ufaulu wa masomo ya sayansi wanafunzi wa shule hizo.
Mwisho.





TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top