Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

Waziri Mkuu Atangaza Neema Kwa Wakulima Wa Zao La Muhogo Ruangwa,Mwekezaji Mbioni Kujenga Kiwanda.

TANGAZO

Na Bashiru Kauchumbe,Ruangwa.
WANANCHI wilayani Ruangwa mkoani Lindi wametakiwa kulima kwa wingi kilimo cha zao la muhogo lengo likiwa ni kukuza kipato chao pamoja na  uchumi wa nchi mazingira yatakayosaidia pia kuondokana na tatizo la njaa linalotokana na mabadiliko ya hali ya hewa yanayosababisha ukame katika baadhi ya vijiji wilayani humo.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Mhe Kassimu Majaliwa kwa nyakati tofauti alipofanya Mikutano ya hadhara katika Vijiji vya Kitandi,Nkowe na Namahema.

Alisema kwa sasa  kilimo cha Muhogo  kina faida kubwa kwani wapo wafanyabiashara ambao wanataka kuwekeza katika kilimo hicho na tayari amempata mfanyabiashara wa kigeni ambaye yupo tayari kununua zao la Muhogo katika Mikoa ya Lindi na Mtwara ambapo amewataka  kuongeza kasi ya uzalishaji wa zao  hilo ili kukidhi mahitaji ya Mwekezaji huyo ambaye amekubali kuja kujenga kiwanda cha kusindika zao la muhogo.

Kwa mujibu wa waziri mkuu amesema kuwa huu ni wakati wa wananchi wa wilaya ya Ruangwa kubadilika na kufanya kazi ili weweze kuendana na kasi ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk.John Pombe Magufuli..

Kwa miaka ya hivi  Karibuni kilimo cha zao la muhogo kilianza kutoweka baada ya wakulima kutoona faida yake huku wakazi wengi wa wilaya ya Ruangwa wakitumia zao hilo kwa ajili ya kupikia pombe wakati wa sherehe mbalimbali za kimila ikiwemo jando na unyago.

 Kwa upande wao baadhi ya wananchi wilayani Ruangwa wamepongeza hamasa na ushauri uliotolewa na Waziri Mkuu huku wakulima wengi wakiahidi  kuwa kwa sasa watachangamkia fursa ya kulima zao la Muhogo kwa kuwa  limekuwa zao la biashara.

Zao la Muhogo kwa mikoa ya Lindi na Mtwara   hulimwa zaidi katika wilaya ya Newala Mkoani Mtwara ingawa kwa sasa  lipo hatarini kutoweka kutokana na wakulima wengi kuacha kulima zao hilo na kukimbilia wilaya za Ruangwa,Kilwa na Liwale mkoani Lindi  kwa ajili ya kulima zao la Ufuta ambalo linaonekana kuwa na soko lenye tija.

TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top