Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

NIMEKUWEKEA HAPA BAJETI YA HALMASHAURI YA MJI MASASI KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017.

TANGAZO
MWENYEKITI wa Halmashauri ya Mji wa Masasi Mh:Sospeter Nachunga (aliyeshika kipaza sauti) akisoma Dua ya Halmashauri kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo. Kushoto kwake ni mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mh:Halima Dendego na Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mh: Bernald Nduta. Kulia kwake ni makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Masasi Mh;Ausi Mnela,mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Masasi Fortunatus Mathew Kagoro na mkuu wa idara ya ukaguzi wa ndani mkoa wa Mtwara. (Picha ya Maktaba)

TAARIFA KWA UMMA KUPITIA VYOMBO VYA HABARI:
BAJETI YA HALMASHAURI YA MJI WA MASASI 2016/2017
Bajeti hii ya Halmashauri ya Mji wa Masasi ya Mwaka wa fedha wa 2016/2017 imeandaliwa kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo:
¨     Sheria ya Bajeti  No: 11 ya  mwaka 2015
¨     Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano awamu ya pili.
¨  Hotuba ya Rais wa awamu ya tano Mh:.John Pombe Magufuli ya Novemba 2015
¨     Ilani ya Uchanguzi ya CCM ya mwaka 2015.
¨   Vipaumbele  vya Halmashauri vikihusisha pia vile vilivyotoka ngazi ya Kata na Vijiji

Halmashauri ya mji wa Masasi inatarajia kutumia fedha kiasi cha Tsh. billioni 19,092,007,820.00

MAPATO:
Katika fedha hizo:
Tsh. Billioni 1, 867,144,000.00 mapato ya ndani sawa na asilimia 9.8.
Tsh. Biliioni 15,925,855,820.00 ni Ruzuku kutoka serikali kuu sawa na asilimia 83.4 ya bajeti  yote ya mwaka wa fedha 2016/2017.
Tsh. Billioni 1,299,008,000.00   ni mchango kutoka kwa wahisani mbalimbali wa nje  sawa na asilimia 6.8 hivyo kufanya kuwa na jumla ya bajeti ya Tsh Billioni 19,092,007,820.00.

MATUMIZI
Katika fedha hizo kiasi cha;
1. Tsh. Billioni 11,384,584,000.00 ni matumizi ya mishahara ya watumishi,ambapo ni sawa na asilimia 59.6 ya bajeti yote.
2. Tsh. Billioni 4,808,636,820 ni fedha za kutekeleza miradi ya Maendeleo ambayo ni sawa na asilimia 25.19.

Bajeti hii ya kiasi cha Tsh billion 19, 092,007,820.00 kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017 imeongezeka kutoka  ile ya mwaka Jana ya Tsh. billioni 16,954,310,834.00 2015/2016 ambayo jumla ni sawa na ongezeko la asilimia 12.6.

MCHANGANUO WA FEDHA ZA MISHAHARA NA MATUMIZI YA KAWAIDA
Tsh. billioni 12,416,227,000.00
1. Tsh. 1,031,643,000.00 ni matumizi ya kawaida (O.C)
2. Tsh. Billioni 11,384,584,000.00 ni mishahara.

MATUMIZI YA MAPATO YA NDANI YA TSH.1, 867,144,000.00.
1.Tshs. 764,359,000.00 sawa na asilimia  40  matumizi ya kawaida
2.Tsh. 186,714,000.00 sawa na asilimia 10  miradi ya Maendeleo ya Wanawake na Vijana.
3.Tsh. 933,572,000.00 sawa na asilimia 50  miradi ya Maendeleo.

MCHANGANUO WA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO
Tsh billioni 4,808,636,820.00
1. Ruzuku (LG-CDG) Tsh. 418,485,000.00
2. Mfuko wa Barabara (Road Fund) Tsh. 2,241,143,820.00
3. SEDP Tsh. 335, 484,000.00
4. Maji (RWSSP) Tsh. 179,513,000.00
5. TASAF Tsh. 579,447,000.00
6. Mfuko wa pamoja  wa Afya (Basket Fund) Tsh. 204,564,000.00
7. Maombi Maalumu
¨     Jengo la utawala  Tsh.750,000,000.00
¨     Miundo mbinu shule maalumu Tsh.100, 000, 000, 00.
                                                                        


MCHANGANUO WA FEDHA KUTOKA SERIKALI KUU TSH: BILLIONI 15,925,855,820.00 sawa na asilimia 83.4.

1. Tsh 11,384,584,000.00 -mishahara ya watumishi

2. Tsh 1,031,643,000.00 matumizi ya kawaida

3. Tsh3, 509,628,820.00 fedha za miradi ya Maendeleo kutoka serikali kuu

5. Tsh 1, 299,008,000.00 ni fedha kutoka kwa wahisani wa maendeleo wa nje.

BAJETI HII IMETOA VIPAUMBELE 07 2016/2017 AMBAVYO NI:
a) Kuwezesha upatikanaji wa elimu bora ya msingi na sekondari kwa kuzingatia usawa
b) Kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo ya pembezoni mwa halmashauri.
C) Kuboresha usafi wa mazingira hasa katika maeneo yenye msongamano kama Kituo cha mabasi na sokoni.
d) Kuimarisha ukusanyaji wa Mapato ya ndani ya Halmashauri na kudhibiti matumizi ya fedha za Serikali za Mitaa na Serikali Kuu.
e) Kurasimisha makazi yasiyo rasmi na kuongeza kasi ya upimaji viwanja kwa ajili ya makazi,biashara,viwanda na maeneo ya kuabudia.
g)Kuongeza wigo wa ajira  na kuboresha hali ya usalama wa kijamii (socio- Protection) hasa kwa wanawake , vijana, makundi maalumu, wazee na watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi.
h) Kukarabati miundombinu ya barabara za Halmashauri

MWISHO:
Aidha katika Makisio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2016/17 Halmashauri ya mji wa Masasi imejikita katika  kutekeleza azma ya serikali ya kutoa elimu ya msingi na sekondari bila malipo kwa kufanya mambo yafuatayo:
·        Kulipa likizo kwa walimu
·        Kugharamia Chakula mashuleni
·        Kulipa gharama za uhamisho kwa walimu
·        Uendeshaji wa ofisi
·        Gharama za mitihani.
Imetolewa na Kitengo Cha Habari na Mahusiano,
Halmashauri ya Mji wa Masasi,
25 April, 2016.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top