Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

Matukio Katika Picha Ziara Ya Naibu Waziri Wa Maji Alipotembelea Wilaya Za Masasi,Nanyumbu Na Nachingwea.

TANGAZO
 NAIBU Waziri Wa Maji Injinia Izack Kamwelwe (Kulia) akitoa maelekezo kwa mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Masasi-Nachingwea (MANAWASA) David Mwamsojo (Kushoto) kwenye moja ya chanzo cha maji cha mradi huo kilichopo katika kijiji cha Nangoo wilayani Masasi wakati wa ziara yake.


 MKURUGENZI wa MANAWASA David Mwamsojo (Mwenye miwani) akimpa maelezo naibu waziri wa maji Injinia Izack Kamwelwe katika chanzo cha mradi wa maji wa Mbwinji alipofanya ziara ya kukagua chanzo hicho cha maji.


 MMOJA wa wananchi wa kijiji cha Nangoo Halmashauri ya wilaya ya Masasi akisoma taarifa fupi kwa naibu waziri wa maji baada ya wananchi wa kijiji hiko kusimamisha msafara wake ili asikilize kero zao.


 NAIBU waziri wa maji Injinia Izack Kamwelwe (kulia) akisisitiza jambo kwa mkuu wa wilaya ya Nanyumbu Sauda Mtondoo katika kijiji cha Masuguru pembezoni mwa mto Ruvuma ambako kutajengwa mradi mkubwa wa maji kwa wananchi wa wilaya ya Nanyumbu. anayesikiliza pembeni ni mbunge wa jimbo la Nanyumbu Duwa Mkuwele.


 MENEJA Mradi wa Ruvuma-Mangaka Water Supply Jones Lukaza (kulia) akitoa maelezo kwa naibu waziri wa maji Injinia Izack Kamwelwe.

NAIBU Waziri wa maji akikagua chanjo cha maji cha Mbwinji anayeoongoza mbele ni mbunge wa jimbo la Masasi Rashid Chuachua.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top