Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

AGIZO LA RC LAANZA KUTEKELEZWA,WAZAZI 23 WATIWA MBARONI 19 KATI YAO WATUPWA RUMANDE

TANGAZO
Na Clarence Chilumba,Masasi.
Wazazi wapatao 23 wakazi wa kata za Mpindimbi na Lukuledi wilaya ya Masasi mkoani Mtwara wamepandishwa kizimbani kujibu shitaka linalowakabili la kushindwa kupeleka watoto wao shuleni waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo wa 2014/2015.

Watuhumiwa  hao wamefikishwa katika mahakama ya mwanzo ya Lisekese hii  leo  jumatatu kujibu shitaka hilo walilotenda kwa makusudi huku wakijua ni kosa linalokwenda kinyume na sheria ya mtoto ya mwaka 2009.

 Mbele ya hakimu wa mahakama ya mwanzo ya Lisekese watuhumiwa 20 walikiri kosa hilo huku watatu wakikana shitaka hilo ambao kwa mujibu wa sheria kesi yao itaendelea kusikilizwa.

Katika shitaka hilo la kushindwa kutimiza majukumu yao kwa watoto wao ikiwemo elimu watuhumiwa 19 wametupwa rumande huku wanne wakipewa dhamana.

Hakimu wa mahakama ya mwanzo ya Lisekese alihairisha kesi hiyo hadi machi 25 2015 itakapotolewa hukumu yake huku watuhumiwa hao 19 wakibaki rumande.

Kufikishwa mahakamani kwa wazazi hao kumekuja ikiwa ni utekelezaji wa agizo alilolitoa mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendego wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa maabara aliyoifanya wilayani Masasi ambapo aliwaagiza watendaji wa kata,vijiji na mitaa kuhakikisha kuwa watoto wote wanaripoti shuleni.
Mwisho.


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top