Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO
MWALIMU MKUU MATATANI UJENZI WA MAABARA
Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara Andrew Mtumusha amemuagiza mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kumchukulia hatua za kinidhamu mkuu wa shule ya sekondari ya kutwa ya Mwenge Mtapika Aziz Mwakalasi kwa kutosimamia vizuri ujenzi wa maabara shuleni hapo.
Aidha  ameagiza kifanyike kikao cha dharula (leo) kitakachomuhusisha mwenyekiti wa bodi wa shule hiyo,mratibu elimu kata wa kata hiyo,ofisa mtendaji wa kata pamoja na mwalimu mkuu huyo ili kubaini sababu za kusuasua ujenzi wa maabara katika shule hiyo.
Pia mwenyekiti huyo alikasirishwa na kitendo cha mwalimu huyo kuondoka shuleni hapo kuelekea mkoani Mtwara bila kuaga kwa uongozi wa Halmashauri na kwamba kitendo hicho ni utovu wa nidhamu.
Mtumusha alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza shuleni hapo iliyokuwa na lengo la kukagua ujenzi wa maabara ambapo alijionea mwenyewe uzembe wa usimamizi unaofanywa na mkuu huyo wa shule.
Alisema miradi mingi katika shule hiyo ikiwemo ujenzi wa nyumba ya mwalimu ambayo hadi sasa haijakamilika utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua mno licha ya Halmashauri kutoa fedha za ujenzi wa miradi hiyo.
Alisema kuwa mwalimu huyo ameshindwa kuendana na kasi ya ujenzi wa maabara hivyo ni dhahiri kwamba hapaswi kuachwa hivi hivi bila kuchukuliwa hatua za kinidhmu ili iwe fundisho kwa wakuu wengine wa shule ambao ni wazembe.
“Kiukweli nimekasirishwa sana na uzembe alioufanya huyu mwalimu, hivyo nakuagiza mkurugenzi haraka iwezekanavyo mwalimu huyu aitwe ofisini kwako ili aje atoe majibu ni kwa nini ujenzi wa maabara hii bado uko kwenye hatua ya msingi wakati fedha tayari ameshapatiwa”Alisema.
Mtumusha alisisitiza kuwa mkurugenzi pamoja na watendaji wake waache tabia ya kuoneana aya na kufanya kazi kirafiki katika kutekeleza majukumu ya kila siku hasa kwa wakati huu ambapo Halmashauri zote nchini ziko kwenye hekaheka ya kutekeleza agizo la Raisi Kikwete.
Kwa mujibu wa Mtumusha alisema vitendo vya uzembe kwa watendaji ndani ya Halmashauri hiyo havina nafasi na kwamba ni vyema sasa wakafanya kazi kwa ushirikiano ili kuondoa migongano ambayo inaweza kujitokeza pale tu wataposhindwa kutimiza majukumu yao.

Mwisho.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara Andrew Mtumusha (Mwenye kofia) akitoa maelekezo mbela ya mafundi wanaojenga maabara kwenye shule za sekondari za halmashauri hiyo wakati wa ziara yake aliyoifanya mwishoni mwa wiki.

Ujenzi wa jengo la maabara linalosuasua lililomtia matatani mwalimu mkuu.

TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top