Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO







CCM YAHAIDI KUSIMAMIA MIRADI
CHAMA cha mapinduzi (CCM) wilayani Masasi mkoani Mtwara kimeahidi kusimamia ilani ya chama hicho katika kuhakikisha inasimamia miradi mbalimbali iliyotekelezwa pamoja na ile inayoendelea kutekelezwa na serikali kuu.
Miradi hiyo ni ile iliyotekelezwa  katika kipindi cha Julai 2013 hadi June 2014 katika sekta ya kilimo,afya,elimu,maji pamoja na barabara na kwamba utekelezaji wake ni kwa kiwango cha asiliia 100.
Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na  mradi wa ujenzi wa daraja la Nangoo ambao umeshakamilika tangu februari 2013 na hadi kukamilika kwake   umetumia fedha za kitanzania shilingi Bilioni 4.9.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na mkuu wa wilaya ya Masasi  Farida Mgomi wakati anawasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010 kwa miradi inayosimamiwa na serikali ambapo amewata wana CCM wilayani humo kuondoa tofauti zao katika usimamiaji wa miradi hiyo.
Kwa mujibu wa mkuu huyo wa wilaya alisema  mradi mwingine uliokamilika ni mradi wa maji wa Mbwinji ulio chini ya Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira  Masasi- Nachingwea (MANAWASA)  uliojengwa na kampuni ya ukandarasi ya M/S Sinohydro Corporation Ltd ya China kwa gharama ya Bilioni 31 hadi kukamilika.
 Akizungumzia kuhusu mradi wa umeme vijijini (REA) alisema kulikuwa na miradi saba ya usambazaji wa umeme vijijini kwa awamu ya kwanza ambapo hadi sasa vijiji saba vya Nanganga,Nangoo,Mkalapa,Mandiwa,Mbuyuni,Matankini Pamoja na Maili sita vimeshapatiwa umeme.
Alisema  ipo baadhi ya miradi ambayo utekelezaji wake haujaanza rasmi kama vile mradi wa  ujenzi wa barabara ya Nachingwea-Masasi-Newala-Tandahimba ambao hadi sasa mkandarasi mshauri  ameshasaini mkataba  na TANROADS makao makuu kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.
Alisema mradi mwingine ambao utekelezaji wake haujaanza ni  mradi wa ujenzi wa nyumba kutoka kwa shirika la nyumba la Taifa NHC ambao tayari Halmashauri ya mji wa Masasi imeshakabidhi eneo la Napupa mjini Masasi  kwa watu wa NHC baada ya kukidhi vigezo ikiwa ni pamoja na kulipa fidia kwa wamiliki wa eneo hilo.
Wilaya ya masasi mkoani mtwara ina jumla ya halmashauri mbili zenye majimbo mawili ya uchaguzi ikiwa na tarafa sita,kata 34, vijiji 176 na vitongoji 903 ambapo kwa sasa pato la kawaida kwa mkazi wa wilaya hiyo ni Tsh.763,0000/= kwa mwaka na kwamba mkakati wa wilaya  ni kufikia kiasi cha Tsh. Milioni 1 kwa mwaka.
Mwisho.                 


TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top