Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO
MKOMAINDO WAZALISHA WATOTO ISHIRINI KRISMASI
Watoto wapatao ishirini wamezaliwa wakati wa mkesha wa krismasi katika hospitali ya mkomaindo mjini Masasi mkesha ambao wakristo kote duniani huadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa  mwokozi wao yesu kristo huko katika mji wa Bethlehemu miaka 2000 iliyopita.
Akitoa takwimu hizo juzi muuguzi wa zamu katika hospitali hiyo ya Mkomaindo Happynes Frank alisema kati ya watoto hao wanaume ni 12 ambapo wanawake ni wanane huku wote wakizaliwa kwa njia ya kawaida.
Alisema hali za watoto hao pamoja na mama zao zinaendelea vizuri na kwamba wengine tayari wamesharuhusiwa kurudi makwao kuendelea na sherehe za krismasi na mwaka mpya.
Kwa mujibu wa muuguzi huyo wa zamu alisema kuwa watoto hao wamezaliwa wakiwa na uzito wa zaidi ya kilogramu mbili ambapo amekiri kuwa changamoto kubwa iliyopo ni kuwa baadhi ya wazazi hao hukosa baadhi ya virutubisho muhimu kwenye miili yao.
Alisema kila mara wamekuwa wakitoa elimu kwa lengo la kuwakumbusha akinamama hao umuhimu wa kupata kinga zote pale wanapokuwa wajawazito pamoja na umuhimu wa kufanya mazoezi na kwamba kwa kufanya hivyo kutasaidia kujifungua kwa usalama.

Mwisho.

MKOMAINDO WAZALISHA WATOTO ISHIRINI KRISMASI
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top