Loading...
ADVERTISE WITH US ON THIS BLOG.CALL +255 714 789 592/ +255 682 997 767/ +255 752 944 022

TANGAZO

KAYA 2944 KUNUFAIKA NA TASAF III HALMASHAURI YA MJI MASASI. 
Na Clarence Chilumba,Masasi
Mpango wa kunusuru Kaya maskini sana kupitia awamu ya tatu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF lll  Halmashauri ya mji masasi mkoani mtwara unatarajia kunufaisha Kaya zipatazo 2944 kati  ya kaya  3035 zilizotarajiwa kunufaika na mpango huo.
Akizungumza na habari leo mjini hapa Mratibu wa Tasaf  Halmashauri ya mji masasi Joram Msyangi alisema utekelezaji wa mpango huo ambao ni kwa mara ya kwanza unatekelezwa hapa nchini ulianza kwa kuzitambua kaya maskini sana kupitia mikutano ya hadhara ilioyofanyika katika kata na vijiji  vilivyoteuliwa.
Msyangi alisema mara baada ya zoezi la utambuzi zilipatikana Kaya  2944  na kila kaya itapatiwa ruzuku isiyo na masharti ya Dola tano kwa mwezi (kama sh.8,500/),na kwamba kwa kuanzia kaya hizo zitapatiwa ruzuku ya miezi miwili.
Mratibu huyo amezitaja changamoto mbalimbali walizokumbana nazo wakati wa zoezi la uandikishaji wa kaya maskini sana kama vile mahudhurio duni kwenye mikutano ya hadhara vijijini  iliyochangiwa na ukosefu wa taarifa pamoja na uwepo wa taarifa za upotoshaji kuhusu zoezi hilo zilizozorotesha mikutano hiyo.
Changamoto zingine zilizotajwa na Mratibu huyo wa Tasaf Halmashauri ya mji masasi ni uelewa duni wa neno maskini hali iliyowafanya wengine wasusie kuingizwa kwenye mpango huo kwa dhana kuwa kuitwa  maskini ni  kitendo cha udhalilishaji.
Aidha ametoa ushauri kwa Serikali kuhusu kaya zilizolengwa lakini hazikuingizwa kwenye mpango huu.”Naishauri Serikali iangalie upya tena namna ya kuweza kuziingiza  kwenye mpango ili walengwa wengi waweze kunufaika kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini sana.”
Halmashauri ya mji masasi ina kata 11 ambapo kati ya hizo  kata kumi ndizo zilizonufaika na mpango huo na zilianza utekelezaji wake kwa kutambua kaya maskini mizunguko minne kisha vilimalizia kwa zoezi la uandikishaji wa kaya maskini kwa mizunguko minne tofauti.

 MWISHO




Wahusika wa mpango huo kwa ngazi ya kijiji wakiwahudumia wananchi

TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by WAYEGE CO.LTD
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mtazamo Mpya | Designed By FAHARI YA TANZANIA
Back To Top